Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Album ya Rick Ross kawashilikisha wakali kibao

Muktasari:

  • Albamu ya Rick Ross itatoka Agosti 9, 2019 ikiwa na nyimbo 15 alizowashirikisha mastaa wakali akiwemo Drake, Jeezy, Swiss Beatz, Meek Mill, Denzel Curry, Ball Greezy na Dej Loaf

Marekani. Rapa Rick Ross ametaja majina ya wasanii watakaosikika kwenye albamu yake ya 10 iitwayo  ‘Port of Miami 2’ itakayotoka Agosti 9, 2019.

Albamu hiyo ni mwendelezo wa albamu ya  ‘Port Of Miami’  iliyotoka 2006 ikiwa na ngoma 15 ikiwamo aliyofanya na marehemu Nipsey Hussle ‘Rich Nigga Lifestyle’ pamoja na Teyana Taylor.

Wasanii wengine watakaotikisa kwenye albamu hiyo ni Drake, Jeezy, Swiss Beatz, Meek Mill, Denzel Curry, Ball Greezy na Dej Loaf.

Kwa mujibu wa tovuti ya RollingStone singo ambazo zinajulikana ni pamoja na  “Gold Roses” aliomshirikisha  Drake, “Big Tyme” aliomshirikisha  Swizz Beatz  na  “Act a Fool” aliofanya na  Wale.