Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wagombea 16 wajitokeza kupambana na Putin

Muktasari:

  • Rais Vladimir Putin anatarajiwa kugombea nafasi hiyo kwa muhula wa tano.

Russia. Wagombea 16 wamewasilisha maombi ya kugombea urais wa Russia mwaka 2024.

Maofisa wa Tume ya Uchaguzi wamesema hayo  leo Desemba 20, 2023, ambapo  Rais wa nchi hiyo,  Vladimir Putin anatarajiwa kugombea kwa muhula wa tano.

 “Tumepokea maombi kutoka kwa wagombea 16 katika uchaguzi wa Rais,” Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (CEC), Ella Pamfilova amenukuliwa na Shirika la Habari la Serikali la Ria Novosti.

Akiwa kwenye mkutano na maveterani wa kijeshi mapema mwezi huu, Putin  aliweka bayana kuwa  atashiriki katika uchaguzi uliopangwa kufanyika mwaka 2024.

Uchaguzi huo utafanyika  kwa siku tatu kuanzia Machi 15, mwakani.

CEC imesema kura pia zitapigwa katika mikoa minne ya Ukraine iliyokaliwa kwa sehemu na vikosi vya Russia na katika rasi ya Crimea, iliyochukuliwa kutoka Ukraine mwaka 2014.

Chama rafiki kwa Serikali ya Russia cha Liberal Democratic wiki hii kilimteua msuluhishi wa zamani wa mgogo wa Ukraine, Leonid Slutsky, kuwa mgombea wake.

Amesema kugombea kwake “hakutaondoa kura” kutoka kwa Putin.

Wagombea lazima wawasilishe maombi ya kushiriki katika uchaguzi wa Machi ifikapo Desemba 27,2023 kwa mujibu wa sheria za uchaguzi.

Baada ya hapo watahitaji kukusanya maelfu ya saini kutoka kwa wafuasi wao ili kupata nafasi kwenye uchaguzi.

Igor Girkin, mtu mwenye msimamo mkali na mkosoaji mkubwa wa Kremlin ambaye yuko kizuizini akisubiri kufunguliwa mashtaka kwa tuhuma za itikadi kali, amesema alitaka kumpinga Putin kwenye uchaguzi huo.

Mwanasiasa wa upinzani aliyefungwa, Alexei Navalny alizuiwa kugombea katika uchaguzi wa mwaka 2018 kutokana na mashtaka ya zamani ya udanganyifu ambayo washirika wake walisema ni ya kisiasa.