Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Trump aigeukia Afrika Kusini, kuinyima misaada

Muktasari:

  • Rais wa Marekani, Donald Trump amesema atazuia misaada kwenda Afrika Kusini kwa kile alichotaja kuwa ni ukatili kwa wananchi wake.

Rais wa Marekani, Donald Trump amesema bila kutaja ushahidi, kwamba "tabaka fulani za watu" nchini Afrika Kusini walikuwa wakitendewa ‘vibaya sana’ na kwamba atakata ufadhili wa nchi hiyo hadi suala hilo litakapochunguzwa.

Trump amebainisha hilo jana, Februari 2, 2025 katika mtandao wake wa Truth akisema kuwa baadhi ya wananchi amekuwa wakifanyiwa ukatili.

"Afrika Kusini inanyakua ardhi, na inawatendea watu wa tabaka fulani vibaya sana," amesema Trump na kuongeza;

"Marekani haitasimama kwa hilo, tutachukua hatua. Pia, nitakata ufadhili wote ujao kwa Afrika Kusini hadi uchunguzi kamili wa hali hii utakapokamilika!" amesema.

Haijulikani ni nini kilisababisha hadi Trump kuchapisha ujumbe huo na hata ulipotafutwa Ubalozi wa Afrika Kusini mjini Washington DC haukujibu chochote kuhusu hilo.

Kwa mujibu wa data ya hivi karibuni, Marekani imetoa misaada ya zaidi Dola milioni 440 Afrika Kusini kwa mwaka 2023.

Mapema Januari, mwaka huu, Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa alisema hana wasiwasi kuhusu uhusiano wa nchi hiyo na Trump. Alisema alizungumza na Trump baada ya ushindi wa uchaguzi na anatazamia kufanya kazi na serikali yake.

Wakati wa utawala wake wa kwanza, Trump alisema Marekani itachunguza mauaji makubwa ambayo hayajathibitishwa ya wakulima wazungu nchini Afrika Kusini na unyakuzi wa ardhi kwa nguvu.


Endelea kufuatilia Mwananchi.