Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ukweli pambano la Mwakinyo, Mghana kukwama uko hivi

Muktasari:

  • Pambano la kuwania mkanda wa WBO lilikwama bada ya mpinzani wa Hassan Mwakinyo kushindwa kutokea licha ya kupigiwa simu.

Dar es Salaam. Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameshindwa kupanda ulingoni kutetea mkanda wake wa WBO Afrika kutokana na mwakilishi wa WBO, Samir Captain kutoka nchini Ghana kushindwa kufika ukumbini.

Mwakinyo usiku wa kuamkia leo alitakiwa kupanda ulingoni kutetea ubingwa wake dhidi ya Patrick Allotey wa Ghana lakini pambano hilo haikuwezekana baada ya mwakilishi huyo wa WBO kugoma kufika ukumbini na maofisa waliotakiwa kuchezesha pambano hilo baada ya kucheleweshewa malipo ya fedha zake.

Mapema jana mchana, Mwananchi lilimtafuta Samir na kumuuliza kama kila kitu kipo sawa kuelekea pambano hilo la ubingwa ambapo alijibu kwa ufupi kuwa kuna mambo yapo sawa na mengine hayapo sawa kwa kuwa bado kuna pesa hawajapewa ambayo hakutaja ni kiasi gani huku akiweka angalizo kuwa kuna asilimia chache za pambano hilo kupigwa.

Lakini usiku wa jana kwenye Ukumbi wa Warehouse uliopo Masaki, mwakilishi huyo ambaye ndiye alikuwa msimamizi mkuu alishindwa kutokea licha ya kupigiwa simu na badala yake aliamua kujifungia hotelini kwa muda wote.

Kutokana hali hiyo, Mwakinyo na mpinzani wake walilazimika kupanda ulingoni na kuongea na mashabiki juu ya changamoto hiyo licha ya kila mmoja kudai kuwa yupo tayari kupigana lakini wamekwamishwa na tatizo hilo.

"Mashabiki wangu, niwaombe radhi kuna jambo limetokea lipo nje ya uwezo wetu japo viongozi wamepambana kulimaliza kwa sababu anayetakiwa kusimamia pambano letu hajafika hapa.

"Niwaombe tuendelee kuvuta subira, nawaomba sana mashabiki wangu msiondoke kwa kuwa mmekuja hapa kwa ajili yangu na nina kiu ya kuonyesha nilicho nacho," alisema Mwakinyo.

Lakini kwa upande wa mpinzani wake alisema kuwa: "Hapa Mwakinyo wala mimi hakuna mwenye makosa kwa sababu sisi tupo tayari lakini kuna mambo ya hovyo ya viongozi ndiyo tatizo hivyo sitegemei kupigana usiku huu kwa sababu mpaka sasa hakuna kinachoendelea".

Baada ya kutoa kauli hizo, mabondia hao walishuka na kuendelea kusubiri kabla ya mwakilishi wa WBO nchini, Emmanueli Mlundwa kuingia ukumbini saa tisa usiku na kufanya kikao kidogo watu wakatawanyika.