Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wataalamu wa afya waonya matumizi tiba mbadala kutibu macho

Muktasari:

  • Kambi ya macho imeanza jana Aprili 18, 2025 , chini ya madaktari bingwa 68 na wataalamu wa afya  iliyoratibiwa na Taasisi ya Tulia Trust kwa kushirikiana na The Bilal Muslim Mission Tanzania.

Mbeya. Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Dk Yesaya Mwasubila amesema  hayo jana Aprili 18, 2025, baada ya Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini Dk Tulia Ackson, kuzinduzi wa kambi ya madaktari bingwa wa macho.

Kambi hiyo ya  siku nne imeratibiwa na Taasisi ya Tulia Trust  kwa kushirikiana na The Bilal Muslim Mission of Tanzania, inayohusha matibabu ya uchunguzi wa macho,upasuaji na utoaji wa miwani.

Dk, Mwasubila amesema asilimia kubwa wananchi wakiona dalili  za awali  ukimbilia kupata tiba mbadala jambo ambalo linaathiri mifumo ya mishipa ya fahamu na kupelekea kupata upofu wa kudumu na uoni hafifu.

"Kuna changamoto wapo wananchi  wanashindwa  kufika Hosptali kutokana na gharama kubwa, lakini wapo wenye  fedha, lakini uingiza imani potofu na kukimbilia kwenye tiba mbadala pasipo kujua athari kiafya," amesema.

Dk Mwasubila ametaja makundi mengine ambayo yako kwenye hatari ya kupata upofu ni  yaliyo athirika na magonjwa ya kisukari na shinikizo la damu.

Wakati huohuo, ameitaka jamii kubadili mifumo ya maisha na matumizi ya vyakula kwa lengo la kudhibiti magonjwa yasiyo ambukizwa ambayo yamekuwa ni hatari na kupoteza maisha ya watu.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya,Dk Yesaya Mwasubila akizungumza na wananchi waliojitoleza kwenye kambi la madaktari bingwa wa  macho. Picha na Hawa Mathias

Spika wa  Bunge na Mbunge Mbeya Mjini, Dk Tulia Ackson ameitaka jamii kutumia fursa hiyo na kwamba  wamepokea madaktari bigwa na wataalam 68 kutoka hosptali mbalimbali nchini.

"Hii ni awamu nyingine,  wamekuja mwaka juzi walifanya uchunguzi wa matatizo ya macho kwa  zaidi ya wananchi 5,000, kati ya hao 260 walifanyiwa upasuaji wa  mtoto wa jicho," amesema.

Mratibu wa kambi hiyo ya macho, Ain Sharrif amesema ujio wao ni kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita na  ombi la Spika wa Bunge Dk, Tulia Ackson ikiwa ni awamu ya pili katika Jiji la Mbeya.

Amesema mambo yanayofanywa na DkTulia ni kutekeleza maandiko ya vitabu vya dini kwa kutoa sadaka kwa kujali afya za wananchi wa Mkoa wa Mbeya.

Mkazi wa Mtaa wa Mabatini, Telezia Kisunga amesema ujio wa madaktari bingwa imekuwa mkombozi kwani idadi kubwa wanakwepa kwenda kupata huduma katika hosptali za serikali  kutokana na gharama kubwa za matibabu.

Kuhusu suala la matumuzi ya tiba mbadala, amesema ni kweli  wengi wanaona ni vyema kukimbilia huko kutokana na ukosefu wa kipato cha kukidhi gharama za matibabu.

Mkazi wa Forest, Peter Fredy amesema kwa kipindi kirefu anasumbuliwa na tatizo la macho lakini amekwama kufika kwa wataalamu wa afya kutokana na ukata.