Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

VIDEO-Daktari bingwa Mtanzania achaguliwa, tuzo za uongozi Ujerumani

Rais mteule wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dkt Elisha Osati

Muktasari:

  • Dkt Osati ni miongoni mwa madaktari watano vijana kutoka Afrika waliochaguliwa katika tuzo za Uongozi katika Utabibu inayoratibiwa nchini Ujerumani.

Dar es Salaam. Rais mteule wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dkt Elisha Osati ni miongoni mwa madaktari watano vijana kutoka Afrika waliochaguliwa katika tuzo za Uongozi katika Utabibu—yaani Young Physician Leaders Award inayoratibiwa nchini Ujerumani.

 

Kutokana na tuzo hiyo, Dkt Osati, ambaye ni daktari bingwa aliyehitimu hivi karibuni katika chuo kikuu cha tiba na sayansi shirikishi(Muhas), ataiwakilisha Tanzania katika mkutano wa afya wa dunia-(World Health Summit) utakaofanyika kuanzia Oktoba 12 huko Berlin.

 

Osati ni bingwa katika magonjwa ya ndani na anahudumu katika hospitali ya taifa ya Muhimbili.

 

Huku nchini Tanzania, aliteuliwa na taasisi ya kitaaluma katika sayansi(Tanzania Academy of Sciences), TAAS, na ni miongoni mwa matabibu 24 vijana watakaoudhuria mkutano wa afya wiki hii huko Berlin.

 

Wenzake waliochaguliwa kutoka Afrika ni Dkt Mohamed Abou El-Enein, kutoka Misri, Dkt Alaaddin Salih kutoka Sudan, Dkt Claudia Silva kutoka Cape Verde and Dkt Sean Wasserman kutoka Afrika Kusini.

 

 Dkt Osati ameiambia MCL Digital kuwa hii ni fursa pekee ya kujifunza uongozi katika Nyanja ya utabibu. Mapema leo hii, emeitembelea kampuni ya Mwananchi Communications Limited na kufanya mahojiano maalumu-VIDEO

 

Amesema hiyo ni fursa ambayo imekuja muda muafaka wakati ambapo  anatarajia kusimikwa rasmi kuwa Rais wa Chama Cha Madaktari Tanzania.