Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Tanzania yasisitiza miundombinu udhibiti usalama wa chakula

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), Irene Mlola (katikati), akizungumza katika mjadala wa ngazi ya juu wa Gulfood World Economy Summit jijini Dubai, Falme za Kiarabu (UAE) leo Jumanne, Januari 27, 2026, kuhusu uhusiano kati ya usalama wa chakula na miundombinu katika dunia iliyounganishwa. Picha kwa hisani ya COPRA

Muktasari:

  • Ushiriki wa Tanzania kwenye Gulfood unaonyesha nafasi ya kimkakati ya nchi katika minyororo ya usambazaji wa chakula kikanda, ukitumia eneo lake kijiografia, upanuzi wa mitandao ya usafirishaji, na ukuaji wa uwezo wa kuhifadhi na kusindika ili kuhudumia masoko barani Afrika, Mashariki ya Kati, na kwingine.

Dar es Salaam. Tanzania inahama kutoka kwenye suluhisho za muda mfupi za usalama wa chakula ili kujenga mifumo endelevu ya muda mrefu, ikisisitiza miundombinu, kanuni na teknolojia za kidijitali kama msingi wa uthabiti wake kitaifa, kikanda na kimataifa.

Hayo yamebainishwa leo Jumanne Januari 27, 2026 na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (Copra), Irene Mlola.

Mlola alizungumza hayo  katika Jukwaa la Uchumi wa Dunia la Gulfood (Gulfood World Economy Summit), sehemu ya Gulfood 2026, mojawapo ya majukwaa makubwa ya kibiashara ya chakula na ushirikiano wa sera duniani.

Mlola amesema Tanzania inatoa kipaumbele katika mifumo inayohakikisha usafirishaji wa chakula unaofaa, salama na uwazi kutoka kwa mzalishaji hadi sokoni.

“Kilimo ni kitovu cha uchumi wa Tanzania, kikichangia asilimia 26 ya Pato la Taifa (GDP), kikiingiza asilimia 30 ya fedha za kigeni, na kuajiri karibu theluthi mbili ya watu,” amesema na kuongeza;

“Kwa kuwa kujitegemea kwa chakula kumezidi asilimia 120, kipaumbele chetu ni mifumo iliyo na muundo, inayotegemea sheria, inayotoa uthabiti, kuaminika na ukuaji.”

Mlola amesema ushiriki wa Tanzania katika Gulfood, unaonyeshwa kupitia banda lake chini ya uratibu wa Copra ukiwa na lengo la kuwaleta pamoja wadau wakuu wa sekta za umma na binafsi.

Katika maonyesho hayo, banda hilo linaonyesha maendeleo katika masoko ya kilimo yenye muundo unaoungwa mkono na vituo vya kisasa vya kuhifadhia, mifumo ya risiti za ghala, majukwaa ya kibiashara kidijitali yaliyodhibitiwa na kanda za usafirishaji.

Kama mdhibiti wa Taifa wa nafaka na bidhaa nyingine, Copra inasimamia ushiriki wa soko, utoaji wa leseni, utekelezaji wa viwango vya ubora, na vigezo vya biashara.

“Muundo huu wa udhibiti umekuwa njia bora ya Tanzania kuondoka kwenye mbinu za biashara zisizo na muundo kuelekea masoko yanayotegemea data na sheria, ambayo yanaunga mkono usalama wa chakula wa ndani na biashara ya kikanda na kimataifa.”

Ushiriki wa Tanzania katika Gulfood pia unaonyesha nafasi ya kimkakati ya nchi katika minyororo ya usambazaji wa chakula kikanda, ukitumia eneo lake kijiografia, upanuzi wa mitandao ya usafirishaji, na ukuaji wa uwezo wa kuhifadhi na kusindika ili kuhudumia masoko barani Afrika, Mashariki ya Kati, na kwingine.

Kupitia juhudi hizo, Tanzania inaweka nafasi yake kama mshirika anayeaminika katika biashara ya chakula duniani, unaochangiwa na uwezo wake mkubwa wa uzalishaji na udhibiti madhubuti, miundombinu ya kisasa, na mwongozo wa sera za muda mrefu.