Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Serikali yasisitizwa kuwachunguza viongozi wa dini kabla ya kuwasajili

Wanawake wa Kanisa la EAGT Calvari Kongowe wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake Wahubiri wa Injili. Picha na Pamela Chilongola

Muktasari:

  • Imeelezwa kuwa wakipewa vibali bila kuhakikiwa wanalichafua kanisa na taasisi ya dini kwa ujumla, kwani baadhi yao hawana wito wa kumcha Mungu.

Dar es Salaam. Chama cha Wanawake Wahubiri wa Injili (WWI) kimetaka kabla Serikali haijatoa kibali cha kuwasajili viongozi wa dini, ijiridhishe iwapo wana wito wa kumtumikia Mungu.

Akizungumza leo Jumapili, Julai 30, 2024 Mkurugenzi wa WWI Jimbo la Temeke, Stella Mabuga amesema,

"Serikali kama itatoa vibali kwa viongozi wa dini kwa kuwachunguza na kuwathibitisha wenye wito wa Mungu, tunaamini matukio ya kulitia doa kanisa au taasisi za dini kwa namna yoyote ile hayatakuwepo.”

Stella amewahamasisha wanawake wawatie moyo wachungaji, waepuke matukio yanayochafua makanisa.

Kinyume na kufanya hivyo, amesema familia zitakosa maadili akitolea mfano watoto wengi kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya.

Naye, Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT,  Calvari Kongowe Privatus Kakweche amesema chama cha WWI kimekuwa kikiwahamasisha wanawake wamche Mungu na kusimamia familia zao.

Amesema baadhi ya familia zipo nje ya maadili hivyo mwanamke anaposimama inasaidia jamii kuwa na watu wema wenye hofu ya Mungu.

"Familia isipokuwa na maadili mema inasababisha watoto kujihusisha na vitendo viovu ikiwemo utumiaji wa dawa za kulevya, wizi, ushoga jambo ambalo linasababisha Taifa kuwa na kizazi kisichokuwa na maadili," amesema Kakweche.