Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Serikali ya Tanzania yashinda kesi Marekani

Serikali ya Tanzania yashinda kesi Marekani

Muktasari:

  • Serikali ya Tanzania imeokoa Dola milioni 55 za Marekani (zaidi ya Sh100 bilioni) baada ya kushinda kesi iliyofunguliwa katika mahakama ya Colombia nchini Marekani na familia ya Vipula Valambhia dhidi ya Tanzania.

Morogoro. Serikali ya Tanzania imeokoa Dola milioni 55 za Marekani (zaidi ya Sh100 bilioni) baada ya kushinda kesi iliyofunguliwa katika mahakama ya Colombia nchini Marekani na familia ya Vipula Valambhia dhidi ya Tanzania.

Hayo yameelezwa leo Jumamosi Aprili 24, 2021 na wakili mkuu wa Serikali, Gabriel Malata mjini Morogoro wakati akifungua mafunzo ya elimu na ustadi wa kazi kwa mawakili wa Serikali.

Amesema uamuzi wa kesi hiyo ulitolewa Aprili 19, 2021 baada ya familia ya Valambhia kushindwa kutokana na hoja mbalimbali zilizotolewa na mawakili wa Tanzania ikiwemo ya familia hiyo si raia wa Marekani na hivyo kukosa sifa ya kufungua kesi nchini humo.

Amebainisha kuwa kesi hiyo ilikuwa inahusu Serikali ya Tanzania kuingia mkataba wa ununuzi wa vifaa  na familia hiyo, na ilitekeleza majukumu yake kulingana na mkataba lakini  familia hiyo iliona kuna upungufu katika utekelezaji wa mkataba huo.

‘’Familia ilichokifanya kwa kile ilichoamini kwamba ni halali kwa upande wao ikaamua kwenda kufungua kesi, katika kufungua kesi huko wakadai kulipwa kiasi cha dola milioni 55 ambayo ni sawa na zaidi ya bilioni mia za Tanzania,” amesema.

Ameeleza  Serikali ilipeleka ushahidi wake kwamba mahakama haikuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi za aina hiyo kwa kuwa wahusika si raia wa nchi hiyo.

Amesema mahakama ya Colombia ikakubaliana na hoja za Serikali ya Tanzania, “baada ya hapo hawakuridhika na kuomba idhini ya kufanya marejeo ya kesi katika  mahakama ya juu ndani ya mahakama za Marekani na hapo Serikali ilipambana nao na kushinda tena.”

Amesema kesi zilizofunguliwa nje ya nchi  zilikuwa nne, kwamba Serikali imeshinda mbili na mbili zinaendelea.