Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Rais Samia mgeni rasmi mkutano wa wakutubi, masekretari

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejinenti ya Utumishi wa Umma, George Simbachawene

Muktasari:

  • Kwa mara ya kwanza mkutano  wa Makatibu Muhtasi na Watunza kumbukumbu utafanyika  Visiwani Zanzibar kuanzia Mei 22 hadi 27.

Dodoma. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan anatarajia kuwa mgeni  rasmi katika mkutano wa Makatibu  Muhtasi na Watunza kumbukumbu   Mei 22 Visiwani Zanzibar.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jumanne, Mei 16, 2023 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejinenti ya Utumishi wa Umma, George Simbachawene amesema kwa mara ya kwanza mkutano huo utafanyika Visiwani Zanzibar kuanzia Mei 22 hadi 27 mwaka huu.

Simbachawene amesema maandalizi kwa ajili ya kikao hicho yamekamilika ambapo zaidi ya wageni 8000 wanatarajia kuhudhuria.

"Nichukue nafasi hii kuwaomba waajiri wote ambako wanachama wa vyama hivi viwili wapo  kuwahudumia kwa  kila kitu," amesema Simbachawene.

Amesema hayo yalikuwa ni maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha anaufanya Utumishi wa Umma unakuwa uliotukuka na unawahudumia wananchi.