Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Jamii lawamani kwa changamoto za wasioona

Muktasari:

  • Wasioona wametakiwa kujiamini katika kila jambo wanalofanya kwa kuwa wana haki sawa na watu wengine wote.

Watu wenye ulemavu wa macho wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo, huku wakibainisha kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni jamii kutotambua haki za kundi hilo.

Wamesema jamii pia haiwatambui, wana ukosefu wa elimu na hudharauliwa.

Msemaji wa Chama cha Wasioona Wilaya ya Kilosa, Juventin Thomas amesema licha ya  chama hicho kuanzishwa mwaka 1964, bado jamii yawasioona inakabiliwa na changamoto nyingi.

Amesema baadhi ya watu katika jamii huwadharau nakuwaona watu wasioona kama wasiofaa na wasioweza kufanya kitu chochote, hivyo kusababisha wakose haki zao zamsingi ikiwamo elimu, kupandishwa vyeo kazini, kukosa semina na mafunzo kazini.

Ofisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Kilosa, Tumaini Geugeu amesema Serikali ya Wilaya ya Kilosa inakitambua chama cha wasioona na inajua kuwa watu hao wanakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinawakwamisha katika kupata haki zao muhimu.

Amesema tatizo lingine lipo kwao wenyewe kwa kuwa baadhi hawajiamini katika kila jambo hivyo kuwepo hatari katika mustakabali wamaendeleo yao.

Mwisho.