Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Haya ni mabadiliko mengine kwa manaibu Waziri

Muktasari:

  • Mabadiliko mengine yafanyika kwenye Baraza la Mawaziri, Mnyeti ahamishiwa wizara ya uvuvi, Silinde aenda Kilimo.

Dar es Salaam. Saa chache baada ya kufanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri Rais Samia Suluhu Hassan amefanya uhamisho na uteuzi kwa manaibu waziri wawili.

Katika uhamisho huo aliyekuwa naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, David Silinde, amepelekwa kutumikia nafasi hiyo katika Waziri ya Kilimo.

Silinde anachukua nafasi ya Alexander Mnyeti aliyedumu kwenye kiti hicho kwa saa chache tangu kuteuliwa akihamishiwa wizara ya mifugo na uvuvi.

Taarifa iliyotolewa leo na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imeonyesha pia kufanyika kwa Balozi Aisha Amour kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi.

Sambamba na hilo Rais Samia amefanya uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Mipango akiwemo

Wajumbe walioteuliwa ni Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu Balozi Ombeni Sefue na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tanesco na Mkuu wa Chuo cha Nelson Mandela Omar Issa.

Wengine ni Balozi Mstaafu na Mjasiriamali Ami Ramadhan Mpungwe  na Meneja Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Cambodia Maryam Salim.