Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Apple yazindua iPhone ya ajabu

Muktasari:

Simu za iPhone 8 na 8 Plus zimeboreshwa kutoka zilizopo za iPhone 7 na 7 Plus kwa kuongeza baadhi ya vitu vinavyopatikana sasa katika bidhaa za kampuni ya Apple.

Kampuni ya Apple imezindua simu mbili za kisasa za iPhone 8 na iPhone 8 Plus jijini California na papo hapo imeitambulisha nyingine ya iPhone X

Simu za iPhone 8 na 8 Plus zimeboreshwa kutoka zilizopo za iPhone 7 na 7 Plus kwa kuongeza baadhi ya vitu vinavyopatikana sasa katika bidhaa za kampuni ya Apple.

Simu ya iPhone X imetengenezwa ikitofautishwa na zingine za kampuni hiyo ambayo ili kuifungua jicho la mtumiaji ndilo litaitambua sura yake.

Oda kwa ajili ya simu hiyo zitaanza kuwekwa Oktoba 27 mwaka huu.

Iphone X haina kitufe ambacho huwa katikati ya simu kwa chini kama zilizo simu nyingine za kampuni hiyo.

Simu hiyo tofauti na nyingine, itachajiwa kwa kutumia vifaa visivyo na waya (wireless) na ukubwa wa kioo umeongezwa katika mfumo wa kisasa.

Iphone X imeongezewa uwezo wa kamera kwa kuwa na 3D, huku ya mbele ina megapix 7 na nyuma megapix 12.

Awali, wabobezi wengi waliamini iPhone 8 ndiyo itakuwa aina mpya ya simu za Apple lakini ni tofauti, kampuni hiyo imetambulisha iPhone X.

Kampuni ya Apple imesema lengo lake siku zote ni kutengeneza kitu cha ajabu na chenye nguvu ambacho teknolojia yake itadumu kwa muongo ujao.