Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mradi wa maji wa Sh119 bilioni chanzo cha Mto Kiwira waanza

Muonekano wa chanzo cha maji katika Mto Kiwira Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya kitakachozalisha lita 117 milioni kwa siku. Picha na Hawa Mathias

Muktasari:

  •  Mradi wa kimkakati wa maji una uwezo wa kuzalisha lita 117 milioni za maji kwa siku

Mbeya. Zaidi wakazi milioni moja wanatarajiwa kunufaika na mradi mkubwa wa kimkakati wa maji kutoka  chanzo cha Mto  Kiwira  Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya ifikapo Machi 31,2025.

Mradi huo utakaozalisha maji lita 117 milioni  kwa siku,  kwa  sasa uko kwenye hatua za ujenzi na usanifu kwa asilimia 98

Akizungumza na Mwananchi Digital Leo Jumamosi ,Mei 18,2024 Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira, Mhandisi Gilbert Kayange amesema utekelezaji wa mradi huo unakwenda kwa kasi kubwa.

"Mradi huu unatekelezwa na mamlaka  kwa  kushirikana na Wizara ya Maji, tunarajia ifikapo   Mei 31,2024  saa 12.00 za jioni  wananchi wataanza kupata majisafi na salama,"amesema Kayange.

Mhandisi  Kayange amesema katika  hatua nyingine  wanaendelea na  ujenzi wa banio kwa kuhamisha mto litakalokuwa na  uwezo wa kukusanya lita  milioni 12 kwa siku.

"Katika  kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati,  tunaendelea na ujenzi wa tenki kubwa la kuhifadhi maji  eneo la New Forest litakalochukua maji zaidi ya lita milioni tano  yaliyotibiwa  tayari kwa ajili ya matumuzi kwa wateja,"amesema Mhandisi Kayange.

Pia, amesema kukamilika kwa mradi huo itakuwa mwarobaini wa changamoto ya huduma ya maji kwa wananchi  Mkoa wa Mbeya.

Akizungumzia uwepo wa mradi huo, Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya, Dourmihamed Issa amesema utakuwa na tija sambamba na  kuchochea  shughuli za kiuchumi kwa  wananchi kutotumia muda mwingi kusaka maji

"Kwanza niishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Mbeya mjini na Spika wa Bunge,Dk Tulia Ackson kuweka msukumu kuwezesha  mamlaka hiyo kupata fedha,"amesema.

Mkazi wa Mamlaka ya Mji wa Mbalizi, Mawazo Adamson  amesema hali ya upatikanaji wa huduma ya maji ni changamoto.