Carbon Tanzania yasherehekea Siku ya Mazingira Duniani kwa kukabidhi hundi ya Sh14.25 bilioni, mapato ya hewa ukaa kwa jamii za Tanganyika

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Phillip Mpango akikabidhi mfano wa hundi ya Sh14.25 bilioni kwa viongozi wa Mkoa wa Katavi na Wilaya ya Tanganyika ikiwa ni mapato ya hewa ukaa kwa jamii za Tanganyika. Makabidhiano hayo yalifanyika wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kilichofan­yika Juni 5, 2024 jijini Dodoma.

Muktasari:

  • Jamii ya vijiji 8 zilizoko ndani ya Wilaya ya Tan­ganyika zimepokea map­ato ya awamu ya nane na tisa ya fidia ya hewa ukaa ya mwaka 2023 kiasi cha Sh 14.25 bilioni, na kupelekea kuwa jumla ya kiasi cha Tsh 22.51 bil­ioni kuanzia kuanzishwa kwa mradi wa milima ya Ntakata
  • Mapato hayo yana­tokana na mkataba na mwekezaji (Carbon Tan­zania) kutokana na shu­ghuli za ulinzi wa misitu ya asili

Vijiji vinane na Hal­mashauri ya Wilaya ya Tanganyika zimepokea mfano wa hundi yenye tha­mani ya Sh14.25 bilioni za Kitanzania.

Mapato hayo yametoka­na na uuzaji wa vyeti vya fidia ya hewa ukaa yenye ubora wa hali ya juu, ili­yoidhinishwa kimatai­fa kwenye soko huria la kaboni ambayo yamepa­tikana kutokana na ulinzi wa Hifadhi ya Misitu kwa kuzingatia mpango wa matumizi bora ya Ardhi ulioandaliwa na vijiji.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Phillip Mpan­go alipokea mfano wa hun­di ya fedha hiyo kwa niaba ya wanajamii katika siku ya kilele cha Siku ya Mazingi­ra Duniani, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikuta­no wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma, Juni 5, 2024.

Mwaka 2017 Serikali za Vijiji ziliingia mkata­ba na mwekezaji mkubwa wa misitu ya asili barani Afrika, Carbon Tanza­nia, kutekeleza mchakato ambao juhudi za ulinzi wa misitu zinatambuliwa kwa kupimwa na kulipwa fidia za kifedha.

Kwa kuzuia ukataji miti katika hifadhi zao za misi­tu, jamii zinachangia kati­ka mapambano ya kimatai­fa dhidi ya mabadiliko ya tabianchi. Misitu inapokat­wa, hewa ukaa husambaa kwenye angahewa na kule­ta athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Hili linapozuiwa kutokea na kusababisha upunguzaji wa hewa ukaa, hutambuli­wa kama utunzaji wa hewa ukaa iliyookolewa kutoka kwenye ukataji wa miti. Carbon Tanzania inauza kiwango kilicho okole­wa kwenye soko la hiari la kaboni (VCM), ambapo mauzo haya huzipa jamii fursa ya kufikia mfumo wa kifedha wa kimataifa.

Jamii za vijiji, kwa kushirikiana na Mamla­ka ya Wilaya, zinapanga mipango ya bajeti na utoaji wa mapato hayo kwa kuzin­gatia malengo ya maende­leo yao na Taifa kwa muji­bu wa kanuni zilizotolewa na Serikali hivi karibuni.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Carbon Tan­zania, Marc Baker alisema “Fidia za mapato ya kifedha kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabinchi ni fursa kubwa kwa Tanzania na kama mwekezaji mkuu katika ulinzi wa misitu ya asili hapa nchini, Carbon Tanzania inalenga kuende­lea kushirikiana na Serika­li ya Tanzania kuwezesha upatikanaji wa fedha kwa ajili ya ulinzi wa misitu.”

Mpango huu unaoongo­zwa na jamii ni kielelezo muhimu cha jinsi jamii za Kitanzania zinavyoweza kulifikia soko la kimatai­fa kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabin­chi kupitia soko huria la kaboni (VCM).

Kuhusu Carbon Tanzania

Carbon Tanzania ni kam­puni ya kitanzania ambayo inachangia katika kukuza uchumi wa nchi na watu wake kwa kutunza misitu asili na viumbe hai kupi­tia uuzaji wa vyeti vya hewa ukaa iliyookolewa na kuwawezesha watanzania kupata mapato kutokana na uhifadhi wa mazingira yao.

Vyeti hivi hununuliwa na mashirika ya kimataifa yenye malengo na mikakati chanya ya kupunguza uzal­ishaji wa hewa ukaa kwa kuwekeza katika shughuli za kiasili zinazochochea na kuleta matokeo bora ya uhifadhi katika utunzaji wa hali ya hewa, jamii na wanyamapori nchini.


Kuhusu mradi wa Milima ya Ntakata

Mradi wa Milima ya Ntakata unasimamia hekta 216,994 za pori la Miombo katika mfumo wa Ikolo­jia wa Mahale, Magharibi mwa Tanzania. Vijiji nane vinavyojumuisha watu 57,189 vinajishughulisha na mradi huu.

Kwa kuendeleza Hifadhi ya Misitu ya Vijiji (VLFRs) jamii hizo zinaweza kulin­da makazi muhimu ya Sokwe wa Mashariki walio hatarini kutoweka. VLFR pia husimama kama kiungo muhimu kati ya mfumo wa ikolojia wa Greater Mahale na Hifadhi ya Taifa kwa Tembo Katavi.

Jamii za wakulima za Bende na Tongwe hulinda msitu wao na thamani ya hewa ukaa iliyohifadhi­wa jambo linalowezesha kuzalisha mapato kutoka­na na mauzo ya vyeti vya hewa ukaa kwa ajili ya kuendesha shughuli zao za uhifadhi kupitia MKUHU­MI (REDD).

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Phillip Mpango (katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa Carbon nchini wakati wa kilele cha maadhi­misho ya Siku ya Mazingira Duniani kilichofanyika Juni 5, 2024 jijini Dodoma. Wa tatu kushoto walioketi ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na wengine ni viongozi wa juu wa Serikali.


Mradi wa MKUHUMI (REDD) umeidhinishwa na VCS na CCB, unazuia miti milioni 1.5 kukatwa kila mwaka na kuepuka tani 550,000 za uzalishaji wa kaboni kila mwaka.


Faida za kimazingira

Kabla ya maendeleo ya mradi huu, ukataji miti katika eneo la mradi uli­kuwa kwa asilimia 3.5, juu ya kiwango cha wastani cha kitaifa cha ukataji miti. Viwango vya ukataji miti vinatarajiwa kupungua sana. Mradi unazuia miti milioni 1.5 kukatwa kwa mwaka.

Mradi huu unalinda Sok­we wa Mashariki walio hatarini kutoweka, Mbwa mwitu, Tai wa Misri na Lappet-faced. Pia hulin­da viumbe walio katika mazingira magumu ikiwa ni pamoja na tembo, pembe za ardhini, Tai wa kijeshi, Twiga, Pangolini, Chui, Simba, White-backed, na Ruppell’s Griffon Vulture walio hatarini kutoweka.


Kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi

Mradi huu unaepusha tani 550,000 za uzalishaji wa hewa ukaa kwa mwaka. Mradi huu hutoa fidia ya hewa ukaa iliyoidhinishwa kwa kulinda misitu iliyo hatarini na utoaji wa fidia kwa kampuni zinazoende­sha miradi ya kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa.

Mapato yanayopatikana kutokana na mauzo ya fid­ia ya hewa ukaa hutumi­ka kulipa mishahara kwa walinzi wa kijamii na viji­ji (VGS), kusaidia mifuko ya afya na ada za elimu, na kufadhili miradi ya maendeleo ya jamii. Mradi huu umeidhinishwa na VCS & CCB ya VERRA, wenye viwango vya kimataifa.