Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

MAPISHI: Jinsi ya kuandaa rosti la uyoga

Uyoga unaweza kutumika kama mboga au supu kulingana na matakwa ya mtumiaji. Pia kama vilivyo vitoweo vingine, uyoga una aina mbalimbali za mapishi.

Leo katika makala haya tutaangalia jinsi ya kutayarisha rosti la uyoga.

Mahitaji

Uyoga robo kilo

Siagi vijiko viwili vya chakula

Kitunguu maji kimoja kilichokatwakatwa

Nyanya mbili zilizosagwa

Kitunguu saumu kilichotwangwa nusu kijiko cha chai.

Pilipili manga ya unga nusu kijiko cha chai

Mafuta ya kula vijiko viwili vya kupakulia chakula

Chumvi kiasi

Jibini kijiko kimoja cha kupakulia chakula

Jinsi ya kutayarisha

Osha uyoga vizuri hakikisha hauna mchanga hata kidogo kwa sababu huwa una tabia ya kutunza mchanga kama haukukaushwa katika mazingira mazuri.

Bandika jikoni sufuria unayotaka kupikia, ikipata moto weka siagi kisha ongeza uyoga na uukaange kwa dakika mbili ili ulainike.

Bandika sufuria nyingine weka siagi ikipata moto ongeza kitunguu maji ukikaange hadi kibadilike rangi kuwa kahawia kisha weka kitunguu saumu na uendelee kukaanga hadi viwe sawa.

Kisha weka nyanya na uache vichemke pamoja kwa dakika mbili, kisha mimina uyoga uliokwisha ukaanga, acha uchemke kwa dakika mbili, kisha ongeza pilipili manga na jibini na uiache iyeyuke na ukoroge.

Hapo rosti la uyoga litakuwa tayari kwa kuliwa na wali, ugali na vitu vingine kama apendavyo mlaji.