Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wazazi wavamia shule wakidhani watoto wanachomwa chanjo ya corona

Wazazi wavamia shule wakidhani watoto wanachomwa chanjo ya corona

Muktasari:

  • Wazazi wageuka mbogo baada ya kuona magari katika Shule ya Msingi Imanga huku wakidhani watoto wanachomwa chanjo ya corona


Kigoma. Wazazi wa watoto wanaosoma Shule ya Msingi Imanga katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, wamezuka shuleni hapo kwa madai ya kuhoji sababu za wanafunzi kupewa chanjo dhidi ya corona bila kupewa taarifa.

Hata hivyo, Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Carlos Mabula amesema leo Jumatano Agosti 11 kuwa wazazi hao waliandamana na kufika shuleni hapo huku wakiwa na hasira ya kudhani ugeni uliofika shuleni hapo ni kwa ajili ya kuchoma chanjo wanafunzi wa shule hiyo.

"Nilitembelewa na wageni ambao ni watalaamu kutoka Tari (Taasisi ya Kilimo Tanzania) waliofika shuleni kwenye shamba  la michikichi ili kujionea hali halisi ya shamba hilo. Hali hiyo ilisababisha mtafaruku  uliolazimisha walimu kuanza kuwatuliza wazazi na kutoa elimu ya chanjo ya virusi vya corona.” amesema Mabula.

Awali, shuleni hapo yalifika magari mawili ya watafiti kutoka Tari kuangalia maendeleo ya shamba la michikichi lenye  mbegu bora aina ya Tenera iliyofanyiwa utafiti na  Tari-Kihinga.


Mmoja wa wazazi hao, Fikiri Waziri amesema kwa kuwa chanjo ni hiari, walimu hawawapi nafasi ya kupata elimu itokananyo na chanjo.

Amesema kitendo cha magari kufika shuleni hapo kimewasababisha wanafunzi kukimbia kurejea  nyumbani kuogopa kuchomwa chanjo.