Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Qnet yawaponza walimu, wafukuzwa kazi

Muktasari:

  • Tume ya utumishi wa walimu wilayani Geita mkoani Geita imewafukuza kazi walimu wanane kwa utoro kazini.


Geita. Tume ya utumishi wa walimu wilayani Geita mkoani Geita imewafukuza kazi walimu wanane kwa utoro kazini.

Walimu hao ambao sita ni wa shule za msingi na wawili wa sekondari, wanadaiwa kujishughulisha na biashara za Qnet badala ya kumtumikia mwajiri huku wengine wakidaiwa kuathiriwa na biashara hizo baada ya kujikuta wanadaiwa na wafanyakazi wenzao waliowaingiza kwenye biashara.

Katibu msaidizi wa tume ya utumishi wa walimu wilayani humo, Sitta Mussanga amethibitisha walimu hao kufukuzwa na kabla ya kufukuzwa tume iliunda kamati ya uchunguzi na kujiridhisha kuwa ni watoro kazini.

“Walimu waliofukuzwa kwa sababu utoro wao umesababishwa na Qnet wako wanane ambao walishatakiwa na waajiri wao kwa nyakati tofauti wapo wa halmashauri ya mji na wengine halmashauri ya wilaya waliacha kazi wakaenda Qnet ambako wanaamini kuna maslahi mazuri kuliko huku kwenye ualimu," alisema Mussanga.

Amesema licha ya kuacha pengo kwenye shule walizokuwa wakifundisha kwa kusababisha uhaba wa walimu pia walikokwenda walichotarajia hawakukipata na baadhi wamepata msongo kutokana na kukabiliwa na madeni.

Akitaja shule zilizoathiriwa kwa walimu wao kufukuzwa, Mussanga alizitaja kuwa ni Kivukoni sekondari walimu wawili, shule ya msingi Nyantorotoro(2), Kivukoni ,Lubanda, Mtakuja na mkoani ambazo zote zimepoteza mwalimu mmoja mmoja.