Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Baadhi ya maeneo ya Dar, Z’bar kukosa umeme

Muktasari:

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi na kitengo cha mawasiliano cha Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) imesema sababu ya baadhi ya maeneo kukosa umeme inatokana na matengenezo ya mashine tatu  za kituo cha Ubungo II

 

 


Dar es Salaam. Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) linawataarifu wateja wake wa Dar es Salaam na Zanzibar kuwa kutakuwa na upungufu wa upatikanaji wa umeme kwa baadhi ya nyakati na maeneo.

Upungufu huo utatokana na kufanya maboresho makubwa yanayohusisha  matengenezo ya mashine tatu  za kituo cha Ubungo II, uwekaji wa transfoma kubwa la MVA 300 kwenye kituo cha kupoza umeme cha Ubungo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Februari 16,2019 na kitengo cha mawasiliano cha Tanesco imeeleza maboresho hayo yanafanyika  ili kukiongezea uwezo kituo cha Ubungo II na kwenda  sambamba na ukuaji wa mahitaji ya jiji la Dar es Salaam  kutakuwa na mapungufu ya upatikanaji wa huduma ya umeme kwa maeneo tajwa.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa  Kampuni ya Songas itafanya matengenezo kinga katika mashine zake ambapo yatakamilika Juni, 2019.

Ilieleza mashine hizo za Ubungo II na Songas zimeungwa katika mfumo wa usambazaji umeme wa msongo wa kilovolti 132 wa Dar es Salaam, Pwani na Zanzibar na hivyo kusababisha mapungufu katika maeneo tajwa.

“Wataalamu  wetu kwa kushirikiana na Mkandarasi Kampuni ya SIEMENS kutoka nchini Sweden wanaendelea na matengenezo  ya mashine na ubadilishaji wa vipuri ili kuongeza ufanisi zaidi katika uendeshaji wa mitambo hii na kuimarisha hali ya upatikanaji umeme kwa Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Zanzibar,” ilieleza taarifa hiyo

“Huduma ya umeme haitakosekana kwa kipindi chote cha matengenezo ila kwa baadhi tu ya siku na nyakati,”.