Baada ya Nawander, mfyatue Bwashee

Juzi mafyatu tulisuuzika roho baada ya kuvuja tuhuma za doktari Yah-yah Nawander kumbaki mwanachuo huko Shimiyu. I just wonder about Nawander. Sitafyatuka mengi. Uchunguzi haujakamilika. Sijui kama kesi iko kwa pilato au la. Tulisuuzika kufyatuliwa wanene wasiofyatuliwa lau kwa kutemeshwa ulaji bila kuwafunga.

Doktari maza alimfyatua Nawander baada ya kutuhumiwa kufyatua Embedodo hadi maganda na kokwa tena kulikooza. Sijui Embedodo liliingiaje mchumani, kama hakukuwa na makubaliano? Je, ni kweli jamaa alikula vyote hata mbegu iliyooza? Yaani mnofu wa Embedodo umeisha hadi fyatu mzima...tena munene na doktari kama wa kweli siyo wa kughushi au honoris cause...unahangaishwa na kokwa chafu?

Huyu udoktari ni wa nini na aliupataje au ni ule wa akina Philo na Sofia? Je, hii ni kweli au kuna namna? Je, usingefanyika usodomu–kama kweli ulifanyika–Embedodo lililoanguka kwenye mchuma wa Nawander–lingelalamika?

Ajabu, nasikia mnaifungia twinter kwa kuhamasisha usodomu wakati wanene ndo wanaoufanya–kama kweli Nawander aliufanya. Je, hawa wanajuana na kukomoana nasi tunafyatuliwa changa la mato au ni siasa kama za kina Sir Baya? Mbona sielewi. Hayo tuyaache.

Leo, kama kawaida ya mshauri wa maza asiyelipwa chochote isipokuwa kusukumwa na ufyatu na uzalendo, natoa ushauri kuntu tena bwerereee. Ushauri wenyewe ni huu. Fyatulia mbali Husaini Bwashee aliyetuhumiwa na Mheshimiwa Luhager Mpiner tena kwa ushahidi kuntu unaoonyesha wazi jamaa alitengeneza uhaba hadi sugar ikageuka shubiri!

Mwe! Mmejua kutufyatua bila kujali tunaweza kufyatuka na kuwafyatua. Kabla ya Mpiner kumwaga mtama, nilikuwa nimehadaika nikatokea kumuona Bwashee mzalendo kumbe wapi? Alivyokuwa akifyatuka na ‘kulaani’ uzembe utadhani alimaanisha! Kumbe sanaa.

Sipendi kufyatua maneno mazito ila naweza kusema hii ni nifakti tosha. Sikutegemea fyatu aliyekuwa anafyatua mapofu 'kuwatetea' wafa kwa ngwamba angekuwa ndiye anayewaumiza mafyatu wa kaya yote.

Doktari Mazeri, naomba nikushauri kumfyatua Bwashee na akina Mwiguuu Nchember, Jan Makamber, na Riz One niliowataja siku zilizopita kwa sababu zifuatazo:

Kwa ushahidi wa Mpiner, kuna kila dalili za upigaji njuluku ndefu kupitia kuongeza cha juu kwenye sugar, kutengeneza faida na rushwa kubwa kwa wanene na walanguzi wa sugar vilivyofanywa na Bwashee ukiachia mbali Nchember.

Alipojipiga kifua akitapika urongo mjengoni kuwa si waziri boya kumbe boyo! Je, kuna mawaziri maboya? Kumbe na mtufuku rahis anaweza kuteua maboya kweli? Kuna uboya kuliko ufisadi waziwazi tena wa kutumwa na akina Mood Doweji? Waziri anapogeuka broker, we acha tu apaswa kuwa mikononi mwa Takokuru kama siyo kunonihino kwenye debe lupango aungane na Nawander.

Pili, kudanganya kaya na mjengo aliojifanya kuuita mtukufu wakati anaufanyia utukutu mbali na kutoa vibali vya kuagiza sugar nyingi kupita naksi iliyokuwapo kayani ni kosa la uhujumu wa uchumi. Ukimsikia jamaa anavyomtaja Sir God, utadhani anamwamini kumbe kamba! Kaya hii kweli ya sanii iko sema Kanjicholi. Haiwezekani umfyatue Nawander kwa masuala binafsi ushindwe Bwashee ambaye skandali yake imeumiza umma wa mafyatu wote.

Tatu, kutoa vibali kwa makampuni feki mengine yakiwa ni ya mamantilie ukiachia mbali la yule bilionea fisadi na uchwara wa kaya. Je, haya makampuni siyo yake au mafyatu wake wapigaji njuluku ndefu ya makapuku wanaofyatuliwa na umaskini tena wa kutengezwa na akina Bwashee, Nchember, na wenzake?

Je, huyu jamaa na wenzake wameishapiga njuluku kiasi gani? Je, wako wangapi kayani? Je, haya huyajui? Kama huyajui, ni kwa nini? Kama unayajua, kwa nini hufyatui? Je, ni kweli unafaidika na akina Bwashee kama mafyatu wapingaji wanavyodai? Je, kwenye bidhaa muhimu kama wese zinapigwa kiasi gani? Je, Nchember na wenzake wameishapiga ngapi? Bandarini nako je? Vipi jamaa wa mbuga za waanimo na utalii? Madini nako vipi? Uhamiaji wajua?

Nne, kusamehe kodi nusu trilioni tena kwa kaya kapuku. Ajabu, wewe maza unatembeza bakuli kukopa na kubomu hadi wengine wanakuita Vasco da Gama kama yule wa Muchoga. Kuna haja gani kudhalilika hivi wakati uchumi tunao ila tunaukalia huku wengine wakiugawa kama huyu Bwashee. Kwanza, kweli huyu ni mdanganyika na mzalendo kweli au ana uraia pacha?

Je, ni wale aliowahi kudai munene mmoja wa geshi kuwa kuna wageni wamepewa nyadhifa kuu kwenye ulaji wa juu? Pili, je, huyu jamaa hawezi kuwa anauza hata siri za kaya na sirkal kwa maadui zetu, wakiwamo magaidi kama vile al Shabubu?

Tano, usipomfyatua, wapingaji wanaaamini kutakuwa na namna unavyofaidika. Wanataja zile pikipiki zilizoandikwa SSH, yaani Sasa Shida Hiyo au Seemingly Self-inflicted Hazard zilizosemekana kugawiwa bure nkoani. Wanadai hizi ndinga zimekula zaidi ya bilioni 50. Je, hii njuluku ilipatikanaje? Zitolewe bure kwani duniani bado kuna cha bure?

Kwa nini sasa kuelekea kwenye uchakachuaji, sorry, uchafuzi, sorry, uchaguzi? Je, nani mwenye hizi ndinga ambaye anaonekana kuwa mkwasi wa kutisha? Pamoja na Luhager kufyatuka kutuhabarisha na kutufumbua mato eti madame Spiker aka Spooker anamtunishia misuli kwa kumpeleka kwenye kamati ya madili wafanyie dili tuhuma zake! Kaya hii kwa maajabu, we acha tu.

Kwa vile nawahi kanywaji, leo nakomea hapa. Hivi nimesema Bashee apandishwe cheo?