Mawaziri wa Fedha wa Afrika Mashariki wamewasilisha bajeti kuu za Serikali zao kwa mwaka wa fedha 2025/26, huku wakikabiliwa na mazingira magumu ya kiuchumi pamoja na mizozo ya kisiasa duniani na katika kanda.
Nchi zilizowasilisha bajeti zao Juni 12, 2025 ni Tanzania, Kenya, Uganda na Rwanda zinazonesha tofauti katika vipaumbele huku zikiweka mkazo kwenye vyanzo vipya vya mapato.
Mwenendo wa bajeti hizo unaonesha kuongezeka mwaka hadi mwaka, huku Kenya ikiwa na bajeti kubwa kuliko nchi nyingine za Afrika Mashariki, ikifuatiwa na Tanzania, Uganda na Rwanda.