Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Magufuli amtaka Majaliwa achape kazi adumu madarakani

Rais wa Tanzania, John Magufuli

Muktasari:

Amemwambia hayo leo alipomwapisha Ikulu ya Chamwino

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania John Magufuli amesema nafasi  aliyompa Waziri mkuu haina uhakika  bali itategemeana na utendaji wake.

Ameyasema hayo leo katika hafla ya kumwapisha Waziri mkuu, Kassim Majaliwa sambamba na Waziri wa fedha na Mpango, Philip Mpango na   Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi iliyofanyika Ikulu Chamwino jijiji Dodoma

Amesema amekuwa akisikia baadhi ya watu na vyombo vya habari vikisema Waziri mkuu Kassim Majaliwa amechaguliwa kuongoza kwa miaka mitano mingine, huku akibainisha kuwa utendaji kazi wake ndiyo utakao mweka katika nafasi hiyo.

“Kwa hiyo tumuombee ili angalau afikie rekodi ya Sumaye (Waziri Mkuu mstaafu) miaka mitano aliyo na guarantee (uhakika) nayo ni aliyomaliza. Hii mingine ni propability (haina uhakika), amesema na kuongeza:

“Na mawaziri niliowateua na nitakaowateua hawana ‘guarantee’ (uhakika) kwa sababu sisi tumezunguka kuahidi kuwa wananchi kupitia Ilani ya chama na wametuamini kwa kura nyingi, imani yao lazima iendane na tutakayofanya, tuilipe, tuitimize kwa nguvu zote,”amesema.