Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wakristo kuadhimisha Ijumaa Kuu leo

Muktasari:

Pasaka huadhimishwa ikiwa ni kumbukumbu ya mateso ya Yesu, huku viongozi wa dini wakihimiza upendo, msamaha na utu wema.

Dar es Salaam. Ijumaa Kuu huadhimishwa siku moja kabla ya Sikukuu ya Pasaka (kufufuka kwa Yesu),  hivyo leo Wakristo dunia wanaadhimisha siku hiyo.

Pasaka huadhimishwa ikiwa ni kumbukumbu ya mateso ya Yesu, huku viongozi wa dini wakihimiza upendo, msamaha na utu wema.

Katibu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Padri Raymond Saba amesema Ijumaa Kuu ni siku muhimu ambayo waumini wa kanisa hilo wanakumbuka fumbo la ukombozi kupitia mateso ya Yesu Kristo.

Amesema Pasaka inaonyesha jinsi Mungu alivyo na upendo uliomuwezesha kumtoa mwanaye mpendwa Yesu Kristo kuteswa kwa kupigwa, kubebeshwa msalaba, kuvalishwa taji la miba na kutobolewa na mkuki hadi kufa ili kumkomboa mwanadamu kutoka katika dhambi .

“Hivyo hakuna Pasaka bila Ijumaa Kuu kwa kuwa hapo ndipo tuliona kilele cha upendo wa Mungu kwa wanadamu, sisi,” amesema