Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Sakata la kampuni iliyofutiwa umiliki wa kitalu Arusha lachukua sura mpya

  Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla

Muktasari:

  • Siku moja baada ya Serikali ya Tanzania kuifutia kampuni ya Green miles Safaris Ltd kitalu cha uwindaji wa kitalii cha Lake Natron East, mkuu wa Wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe ameagiza kumarishwa ulinzi katika kitalu hicho.

Arusha. Siku moja baada ya Serikali ya Tanzania kuifutia kampuni ya Green miles Safaris Ltd kitalu cha uwindaji wa kitalii cha Lake Natron East, mkuu wa Wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe ameagiza kumarishwa ulinzi katika kitalu hicho.

Jeshi la Polisi, madiwani na makatibu tarafa wa Longido, Kitumbeine na Engarinaibor ndio waliopewa jukumu la kuimarisha ulinzi huo ili kuzuia mali za mwekezaji hadi pale atakapolipa deni la Sh336 milioni analodaiwa na vijiji 23.

“Nawaagiza polisi wilaya  ya Longido kuhakikisha wanaweka ulinzi wa kutosha wa mali zote zilizopo pale ili zisichukuliwe hadi tuhakikishe ameingiza fedha kwenye akaunti  za vijiji. Vinginevyo tutavitaifisha vitu vyote na kwenda mahakamani ili vipigwe mnada,” amesema Mwaisumbe.

Jana,  Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla alitangaza kufuta kitalu hicho, na muda mfupi baadaye mkurugenzi wa kampuni hiyo,  Awadh Abdallah alisema kitalu hicho hakijafutwa kama ilivyoelezwa na waziri huyo.

Leo Kigwangalla amelionyesha Mwananchi barua yake kwenda kwa meneja wa kampuni hiyo ya Agosti 7, 2019  yenye kumbukumbu namba CBA.177/389/01/281, akimueleza kuwa amefuta umiliki wa kitalu hicho.

Katika maelezo yake ya leo,  Mwaisumbe amesema haiwezekani mwekezaji aje katika maeneo hayo ya wananchi na apewe masharti ya kufuata ikiwemo kuchangia kiasi cha fedha zinazopatikana na kupeleka kwenye vijiji, lakini hatekelezi jambo hilo.

Amebainisha kuwa alifika katika kijiji hicho mwaka 2013 na tangu wakati huo amekuwa hatoi ushirikiano kwa viongozi  wa ngazi mbalimbali wakiwemo wananchi.

Mkazi wa kata ya Mundarara wilayani Longido  na mbunge wa zamani wa Longido, Lekule Laizer aepongeza hatua hiyo ya Serikali kwa maelezo kuwa wamekuwa wakisumbuliwa na mwekezaji huyo.

“Sijawahi kusikia mwindaji anapiga marufuku mifugo kuingia katika eneo la uwindaji wakati eneo hilo ndio ameweka kambi. Anawazuia wananchi kulisha mifugo yao  wakati yeye ndio kawaingilia na bado amekataa kuwasaidia wananchi wanaozunguka eneo hilo,” amesema.

Diwani wa Mundurara, Alais Mushao naye alipongeza uamuzi huo kauli ambayo iliungwa mkono na wananchi wengine akiwemo Millya Kiloriti.