MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Kitaifa Mwinyi atetea ajira za wafanyakazi, ashauri utu uheshimiwe kudumisha Amani
BOOKMARK THIS PAGE
Mwinyi atetea ajira za wafanyakazi, ashauri utu uheshimiwe kudumisha Amani  Send to a friend
Thursday, 06 May 2010 22:46

Na Fredy Azzah:

SIKU mbili baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa hotuba kali na maagizo ya kutimua wafanyakazi wote ambao wangeitikia tangazo la mgomo lililotolewa na Tucta, Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi amesema serikali inatakiwa kulinda ajira za wananchi wake ili kudumisha amani.Rais Kikwete, akizungumza na wazee wa Dar es salaam kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jumatatu iliyopita, alisema mgomo huo ulioandaliwa na Tucta ni batili na kwamba, yeyote ambaye angehusika, angechukuliwa hatua za kisheria; ikiwa ni pamoja na nguvu ya polisi kutumika kuwazuia watakaoingia mitaani kuandamana.

Katika hotupa yake Kikwete alisema viongozi wa Tucta kuwa ni wazandiki, waongo, wanafiki na wafitini kwa kuwa wanakwenda kinyume na makubaliano yao na serikali.  

Lakini jana Mzee Mwinyi alionyesha mtazamo tofauti jana katika hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Shule ya Kimataifa ya Wavulana ya Feza, ambako alitoa somo fupi la dhima ya utu.

"Taasisi au nchi yoyote ambayo itakuwa haiheshimu utu wa wananchi wake, itakuwa inajichimbia kaburi," alisema Mwinyi kwenye hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na mtoto wa mfalme wa Norway, Haakon Magnus na baadhi ya viongozi wa nchi mbalimbali.

"Ni lazima kwa serikali yoyote ile kuwalinda watu wake na si kufanya uadui kati yake na wananchi. Serikali yoyote duniani ni lazima ilinde ajira za wananchi wake ili iweze kudumisha amani na kuheshimu utu wa raia wake."

Hotuba ya Rais Kikwete ilitafsiriwa kuwa ni ya vitisho na ambayo ilitolewa bila ya ushahidi wa kutosha kutoka pande zote mbili kuhusu maendeleo ya mazungumzo baina ya serikali na Tucta, ambayo ilieleza baadaye kuwa rais alipaswa kwanza kusikiliza viongozi wa shirikisho hilo badala ya kusikiliza watendaji wa serikali pekee.

Mgomo huo ambao ulipangwa kuanza Mei 5, umesogezwa mbele hadi baada ya Mei 8, siku ambayo serikali na Tucta watakutana kujadili suala la kima cha chini cha mshahara wa sekta ya umma, suala ambalo hadi sasa pande zote hazijafikia muafaka.

Mbali na haki ya ajira, Mwinyi pia alisema haki ya kuishi lazima ilindwe na serikali ili kuweza kudumisha amani na kuheshimu utu wa watu wake.

“Vitu kama uhuru wa kujieleza, kusali,  mawasiliano lazima vipewe ruksa, lakini pia ajira na kuishi, haki hizi lazima zilindwe na serikali,” alisema Mwinyi.

Kauli hiyo ya Mwinyi imekuja wakati kukiwa bado na kutoelewana baina ya serikali na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta) lililositisha mgomo uliopangwa kuanza Mei tano mwaka huu, baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa hotuba kali ambayo wadau mbalimbali walisema ilikuwa imejaa vitisho.

Mbali na hayo Mwinyi alisema: “Shule ya Feza ni nzuri sana, ni nzuri kwa sababu ina walimu wazuri na hata wanafunzi wake ni wazuri, hata katika matokeo yake imekuwa ikifanya vizuri na kuwa ndani ya shule tano bora.”

Kabla ya kutoa hotuba yake, baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo walieleza kwa nyakati tofauti juu ya maana ya utu kutokana na mafunzo waliyopata kutoka kwa viongozi hao wa vijana wa dunia.

Watu mbalimbali, akiwemo mtoto huyo wa mfalme wa Norway walikuwa wakihamasika na kuwashangilia wanafunzi hao walipookuwa wanaeleza maana ya utu, umuhimu wa kuheshimu utu wa mtu na athari zake endapo hautaheshimiwa.

Prince Haakon aliwaambia vijana hao ni muhimu kuheshimu utu na kujiamini kwa kuwa wao ndiyo watakaoweza kuifanya Afrika na dunia kwa ujula kuwa mahala pazuri na salama pakuishi.

Baadhi ya wanafunzi hao wakizungumza mbele ya Mzee Mwinyi walisema "utu ni kuheshimiana baina ya mtu na mtu; kusema ni sisi na si ni mimi, kujiuliza nimetoa nini na siyo nimepokea nini".

Wengine pia walisema, kujilimbikizia mali nyingi si utu na kuwa hata mtu huyo aliyejilimbikizia mali wakati anazungukwa na watu masikini haishi maisha ya amani kwa kuwa wale wasio nacho nao watakuwa wakifanya kila liwezekanalo kupata mali za mtu huyo tajiri.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Saturday, 08 May 2010 10:28
 

Comments 

 
0 #65 2012-01-23 14:39
Ni vyema kutoa maoni , lakini izingatiwe pia kuwa mtoa maoni huyo huyo maoni yake yanaweza kutolewa kasoro pia. inashauliwa na wahenga kutumia safu ya maoni kwa kujenga hoja kwa kutumia vigezo ustaarabu na ushauri ukilinganisha na uzoefu uliopo kwenye maeneo mengine. kumejitokeza safu ya maoi kutumika kuchafua viongozi, kutoa mambo yasiyo na ushahidi. kufanya hivyo tunakinzana na kuheshimiana tulikokuzoea Watanzania . "ulionapo kosa ni wewe inawezekana si kosa kwa wengine" KILA LA HERI. mungu atubariki sote
Quote
 
 
0 #64 2010-05-09 13:44
KUNA WACHANGIAJI WWENGINE KAMA BIZZLE inaonekana ni MVIVU WA KUFIKIRI NA KUELEWA MAMBO HIZO POINTI ZAKO KATOLEE SEGEREA NYIE NDIO MNAIFANYA INCHI IWE MASIKINI.KWANI UMEFIKA DARASA LA NGAPI?
Quote
 
 
0 #63 2010-05-08 11:39
kauli hizi za kikwete inathibitisha wazi kuwa ccm ni chama cha mafisadi na si chama cha wafanyakazi tena. wafanyakazzi wanaomba nyiongeza ya mshahara wanatishiwa jela na kufukuzwa kazi wakati watu wanaiba mabilioni wanapigiwa magoti na kuombwa kurudisha pesa bila hata kwenda jela japo kwa siku moja. hii inathibitisha wazi kwa ccm si tena chama cha wafanyakazi bali ni chama cha mafisadi maana kama kauli kama hizi kikwete angezitumia dhidi ya mafisadi wa nchi hii tungekuwa mbali sana lakini anazitumia dhidi ya wanyonge.
Quote
 
 
0 #62 2010-05-08 10:36
Napenda sana kusoma maoni kuhusu habari mbalimbali LAKINI lugha za [NENO BAYA] si nzuri. kuna watoa maoni ambao sio wastaarabu ktk kutoa maoni yao. naomba wabadilike. kumbuka, wasomaji tulikuwa na nafasi ya kutoa maoni ktk gazeti la tanzania daima lakini nafasi hiyo ilitolewa sababu wa wasomaaji wasio wastaarabu. Naomba msituaribie ktk Mwananchi. pia naomba mhariri mwananchi afute maoni yote yosiyo ya kistaarabu.Asante
Quote
 
 
-1 #61 2010-05-08 09:34
Ndugu Mhariri wa maoni, neno baya ni lile lilioandikwa likijitegemea. Lakini sehemu ya neno isitenganishwe kwenye neno ikaitwa neno baya. Hapana. Ninaomba mfeed upya monitor yenu maneno yenye mwambatano unaoupa maana neno zima e.g. tofauti, kuwa tofauti, ukitaka kusema utofauti wa vitu viwili, sehemu ya neno hilo mnalihakiki kama 'neno baya'. Kwa vipi?
Quote
 
 
+1 #60 2010-05-08 09:30
Maoni ni mengi na yanatofau[NENO BAYA] kwa sababu mitazamo pia ya kiitikadi inatofau[NENO BAYA]. Lakini ukweli utabaki ukweli tu: Rais Kikwete hastahili kuwa Rais wa nchi. Rais hasemi maneno ya hovyo kwa wananchi wake. Rais ni mtu makini, mwenye busara na weledi uliotukuka kuliko mwananchi mwingine ye yote. Ikulu amefuata sifa za kuitwa Rais, si saizi yake. Wasaidizi wake wanamdhalilisha kila uchao, hakemei hilo. Ila la wananchi wake kutaka maisha bora aliyoahidi, anawakashfu na kuwatishia. Simwelewi!
Quote
 
 
-1 #59 2010-05-08 03:30
Quoting Mondulijuu:
MIE NAONA WASOMAJI WOTE HAPA NI WANASIASA NA TENA WOTE WA UPINZANI MSIO NA LOLOTE WALA CHOCHOTE. HIVI NYIE MLITAKA RAIS AWAPIGIE MAGOTI? AU MLITAKA ALIE? KABLA YA HAPO ALIONGEA KWA UPOLE KABISA NA KUWASIHI HAWA MANDUMILAKUWILI WAACHE KUCHOCHEA CHUKI LAKINI KWA VILE WALIKUWA NA LAO JAMBO BASI IKABIDI SASA MAMBO YABADILIKE. UKIOMBWA KUINGIA GERESANI SIO KWAMBA UNAOGOPWA BALI SLAHI TU. UKIKATAA MZEE MATEKE UTAPATA VIZURI SANA. HAWA TUCTA WARUDI KWA WALIOWATUMA KUMBIB RAIS KUWA SASA RAISI KAWAPIGIA MBONA HAWATAKI KUPOKEA. HAMNA MAANA KABISA NINYI?

WEWE NDO UMEPOTEZA DIRA KABISA
Quote
 
 
0 #58 2010-05-08 00:30
ndugu mhariri mbona nimetaja kabila lakini matuambia ni neno baya, hi safu yetu tunaiheshimu sana tu.ni safu ilyoandaliwa kiumakini mkubwa na 95% ya wachangia hoja ni watu makini sana. unaweza kuktutafutia neno mbadala ya kulitaja kabila letu hili?nadhni utakuwa umelifahamu.
Quote
 
 
0 #57 2010-05-08 00:21
mwananzengo,hil o ni neno la kisu[NENO BAYA] lakini unatuaibisha wasu[NENO BAYA] wenzako.huoni hata aibu,unashabiki a ccm kama mshabiki wa simba na yanga.hakika wewe umechelewa,we unaona raha gani kula kuku kila siku wakati jirani yako analala njaa? jaribu kusoma vitabu vya dini uone kama yafanywayo na viongozi wa ccm pamoja na ushabiki wako kama vina baraka za mwenyezi mungu.Kikwete hatufai,kama angekuwa muungwana angeachia madaraka kwa kushindwa kutekeleza matazamio ya waTz hata kwa5%.akubali tupige kura za kutokuwa na imani nae kama anajimini.Quoting Mwananzengo:
Tunaweza kuongea mengi kupitia safu hii lakini haingii akilini eti CCM itang'onelewa na Wapinzania miezi 4 na nusu ijayo ni ndoto ya mchana! Ni rahisi kumng'oa JK kuliko ilivyo vigumu kung'oa jitu liitwalo CCM. Hivi wananchi wangapi waliopata fursa ya kuisikia hotuba ya Rais? Bila shaka wengi hawana habari ambao ndiyo watakao 'tia kura zao kwa moyo mmoja!'. Hii ndiyo habari kwa taarifa yenu mnaodhani CCM itashindwa.
Quote
 
 
0 #56 2010-05-07 21:13
JK ameshindwa kuongoza nchi ndio maana anatetea Mafisadi wenzake. hata watanzania mnaopenda CCM sasa mmshapata jibu lenu, Rais gani Jeuri kwa raia walimpa kura? Watanzania tunahitaji leader mwenye kupenda nchi na wananchi sio Mtawala safari bado ndefu ya kumfukuza Mkoloni CCM. Watanzania tushikamane ili tumuondoe huyu mkoloni anayekula Kodi zetu bila ya kujali nchi wala raia
Quote
 
 
+1 #55 2010-05-07 20:29
Mondulijuu mimi ni Mtanzania ambaye sijawahi kujishughulisha kwenye mambo ya siasa, lakini miaka inavyozidi kwenda ndio naona jinsi maisha ya watanzania wengi yanavyozidi kuporomoka huku mafisadi wakizidi kujilimbikizia mali. Hii sio haki kabisa, leo hii Kikwete na viongozi wenzake wanajilipa mishahara mikubwa na kujilipa "per diem" za safari ambazo hazina faida yeyote katika maendeleo ya nchi yetu. Hebu zunguka Tanzania ujionee mwenyewe wananchi wa kawaida wanavyoteseka kimaisha, Ni yeye Kikwete alietakiwa ahakikishe kuna miongozo mizuri ya wananchi kujiajiri au ahakikishe kuna mipango endelevu ya uzalishwaji wa ajira kwa wananchi wake. Hatuwezi kuendelea kukaa kimya, hatuwezi kunyamazishwa tena. CCM inanuka rushwa na inanuka Ufisadi. Kikwete na CCM yake hawafai.
Quote
 
 
+1 #54 2010-05-07 20:23
Sawa Johari,
Ningependa sana nchi iendeshwe hivyo bila tabasamu kwa akina Chenge waliotuingiza katika mikataba ya kifisadi, akina Karamagi, wauaji wa maalbino, wanaochapachapa walimu na wasiowalipa mishahara yao na nauli,mawaziri wanatumia nafasi zao vibaya na wale maafisa wa ikulu waliotaka kuwapa gari la Monduli watu wa Morogoro, na sio kwa watanzania waliokuwa wanaomba angalau wapewe shilingo elfu 10000za kuwasomeshea watoto wao katika shule za kata. Joharo mimi sikuelewi kabisa na wala sielewi kitu gani kinakufanya ushangilie.
Hivi unajua kuwa mwaka huu kila mbunge akimaliza, licha ya milioni 12 za kila mwezi na maalawansi kibao, atapata sh milioni 40 za kustaafu, na atakapokwenda jimboni atapewa milioni nyingine 40 ya kupiga kampeni na bado unashangilia kuwa rais amekuwa mkali na anatakiwa kuwa hivyo. Rais amekuwa mkali wakati na mahali pasipofaa, kwa kuwa hakusoma nyakati. Wafa
Quote
 
 
+1 #53 2010-05-07 20:11
Monduli,

suala si CCM , wala si kura anazoomba kikwete , sababu akina monduli wengi wanaoona mambo ni salama watampa kura hataa kama baba, mama na watoto wao wata teseka katika nchi hii yenye maziwa na asali. Suala ni hotuba mbaya ya Rais iliyokosa usikivu na uvumilivu. Rais hana huruma kwa watanzania wanaopata dola 77 (sh 104000) kwa mwezi, wakati wabunge wanapata dola 8888 (sh12,000,000/=).Suala ni maombi yao ya tangu mwakaa 1990 ya kupewa sh 315,000/= (dola 290 tu) Ili wale ugali na maharage kwa siku 30.Nadhani kama umesoma utajua kuwa wanataka kupewa angalau sh 10,000 tu kwa siku kwa familia ya watu sita. Suala la kura na sisiem halipo ni suala la Raisi kutokutumia vizuri cheo chake kuwasaidia walalahoi badala yake anawatisha na kuwakejeli. Monduli mimi sikupendi na sipendi kauli zako wala sitaki kukuona.
Quote
 
 
-4 #52 2010-05-07 20:04
SAFI SANA RAISI KIKWETE HIVYO NDIO UNATAKIWA KUFANYA TOKA AWALI NCHI HAIENDESHWI KWA TABASAMU
Quote
 
 
0 #51 Administrator 2010-05-07 18:24
Quoting Jamili:
MHARIRI COLUMN HII ITAKUWA NA MAANA TU PALE UTAKAVYOHAKIKIS HA ZINAWAFIKIA HAOOOOOOOOOOOO JAMAA< WANAOWASHABIKIA WAMEKATA TQAMAA AU WANAFUATA MKUMBO.MBONA MAJIRANI ZETU HATUONI TATIZO HILI HIZO ZIARA ZA NJE ZA VIONGOZI ZIWE ZA KUJIFUNZA NA SIO UTALII, WAKITAKA UTALII WAENDE HIFADHINI KWETU.

Jamili, napenda kukuhakikishia kwamba maoni yenu yanawafikia walengwa. Kama nilivyokuwa nimeahidi kuhusu kuweka gazetini maoni yenu kwenye ile story ya bibi kizee kupinga hotuba ya JK, nilifanya vivyo. Na pia tulipiga simu ikulu kuhakikisha pia kwamba wanayaona maoni hayo.

Ninachowaomba tu ni kuwa wastaarabu na kutumia lugha safi. Yaliyobakia niachieni mimi.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner