MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Kitaifa Bi kizee asafari kilometa 50 kupinga hotuba ya JK, AMUONYA ASITUMIE MADARAKA YAKE VIBAYA
BOOKMARK THIS PAGE
Bi kizee asafari kilometa 50 kupinga hotuba ya JK, AMUONYA ASITUMIE MADARAKA YAKE VIBAYA  Send to a friend
Tuesday, 04 May 2010 23:13

Emerentiana Masondole na Salim Said
 
WAZEE zaidi ya 1,000 waliokuwa wakimsikiliza Rais Jakaya Kikwete juzi kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee walikuwa wakimshangilia mara kwa mara, lakini si Bi Asha Omary, 70, aliyekuwa kijijini kwake wilayani Kisarawe.
Kikongwe huyo alisikiliza hotuba hiyo, iliyobatilisha mgomo wa wafanyakazi uliopangwa kuanza leo, kwenye redio akiwa Kijiji cha Bwana, Kata ya Kibuta na hasira alizopata kutokana na kauli za rais, zilimfanya aamue kusafiri takriban kilomita 35 kuanzia saa 1:00 asubuhi kuja jijini Dar es salaam kueleza jinsi alivyokerwa.

“Kama kiongozi wa taifa, rais angetumia maneno ya busara na hekima yasiyo na ukali ndani yake katika kutatua tatizo kwa sababu wafanyakazi wanadai haki yao na wanayo haki ya kufanya hivyo,” alisema Asha alipofika ofisi za gazeti la Mwananchi majira ya saa 4:30 jana.

“Rais amejisahau na anatumia vibaya mamlaka aliyopewa na Watanzania kuwakandamiza wafanyakazi, amesahau kuwa nafasi hiyo imetokana na wananchi wote wakiwapo hao wafanyakazi.”

Bi Asha alikuwa akizungumzia hotuba ya Rais Kikwete kuhusu mgomo wa wafanyakazi uliopangwa kuanza leo, hotuba ambayo iliwashambulia viongozi wa Tucta kuwa ni "waongo, wanafiki, wazandiki na wafitini" kwa madai kuwa wamekuwa hawawaelezi wanachama wao kuhusu maendeleo ya mazungumzo baina ya pande hizo.

Katika hotuba hiyo ya dakika 95, ambayo pia ilirushwa moja kwa moja na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1), TBC Taifa na redio Uhuru, Rais Kikwete, ambaye alikuwa akishangiliwa mara kwa mara na wazee hao ambao wengi walivalia mavazi ya rangi za njano na kijani, alitangaza mgomo huo kuwa ni batili kwa mujibu wa sheria za utumishi wa umma.

Bi Asha, ambaye ni mkulima wa jembe la mkono, alisema rais hakutumia hekima na busara katika kutatua kero za wafanyakazi bali alitumia cheo chake kuwatisha wafanyakazi katika kutetea haki zao.

Alisema kwamba serikali inapaswa kuweka umuhimu wa kutatua kero za wafanyakazi kwa kuwa ndio wanaotoa huduma zote muhimu kwa wananchi wote hasa masikini ambao ni wakulima.

Alisema rais na familia yake wanatibiwa nje ya nchi ndiyo mana haoni umuhimu wa kutatua kero za wafanyakazi badala yake anatoa majibu ya dharau kuwa kama hawataki kufanya kazi waache.

“Au kwa kuwa rais na viongozi wenzake wanatibiwa Ulaya na Marekani ndio maana anatoa vitisho au anataka uwe kama mgomo wa mwaka juzi kwenye Hospitali (ya Taifa) ya Muhimbili ambako watu walipoteza maisha,” alihoji Asha.

“Kama wafanyakazi nao wakisema liwalo na liwe wakachukua hasira kama alizochukuwa rais, itakuwaje; madaktari, manesi na watumishi wengine wakigoma, je haitasababisha maafa kwa Watanzania?”

Asha ambaye alitumia muda wa dakika 70 kueleza masikitiko yake, alisema wakati rais anawatisha wafanyakazi ili wasigome, anapaswa kufunga safari kwenda maeneo ya vjijini kujionea hiyo misaada ya matrekta na ‘Power Tiller’ kama imewafikia wananchi au inatumiwa na viongozi wa vijiji kwa maslahi yao.

Rais katika hotuba yake alisema serikali haiwezi kulipa kima cha chini cha Sh315,000 kwa watumishi wa umma kwa sababu wananchi wengine watakosa huduma za afya, pembejeo za kilimo na hata vifaa vya elimu na walimu.
“Sisi wakulima hatuwezi kugoma lakini kwa muda mrefu hata hizo pembejeo na matrekta anayoyazungumzia hatuyaoni, mbona hachukui hatua na kutoa hotuba kali kwa maafisa wake ili na sisi tupate hizo pembejeo,” alihoji Asha ambaye ni mtoto pekee katika familia yao.

“Sisi vijijini hatuna huduma bora za afya, maji, barabara, shule na rais anasikia kila siku Watanzania wakilalamikia hali hiyo. Je kwa nini rais asitumie cheo chake kuchukua hatua kutatua matatizo ya wananchi kama alivyoamua kwa wafanyakazi,” alisema Asha kwa hasira.

Akizungumzia kupanda kwa gharama za maisha, Asha alisema enzi za utawala wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, bei za vyakula zilikuwa zinafanana katika maduka yote, lakini sasa kila mfanyabiashara ana bei zake.
“Je serikali inashindwa kusimamia tatizo la kupanda kwa gharama za maisha au rais anawaogopa wafanyabiashara... na kama anawaogopa itakuwaje kwa Watanzania,” alihoji Asha.“Namuomba rais siku moja angalau afanye ziara ya kupita katika maduka na kuhoji au kuangalia bei za vyakula halafu alinganishe na vipato vyetu sisi Watanzania kama tunamudu.”

Katika harakati za kutatua tatizo la ugumu wa maisha yake, bibi huyo alisema alishaenda ikulu mara mbili na kugonga hodi ofisi ya Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (Wama), inayoongozwa na mke wa rais, Mama Salma Kikwete ili kuomba mkopo kwa ajili ya kufanya biashara.Asha alisimulia kuwa alifanikiwa kuonana na mmoja wa watendaji wa Wama na kumuelea shida yake, lakini alijibiwa kwamba fedha za Wama zina mlolongo mrefu na kwamba yeye hawezi kuzipata.

“Nilipohoji ni mlolongo gani, hakunifafanulia ila aliishia kuniambia tu kwamba ni mkubwa na huwezi kupata fedha hizi... rudi nyumbani. Nikamuuliza je hizo fedha mnazotangaza kwamba mnawakopesha wanawake ni wanawake wote au mna wanawake maalum ambao wanastahiki, sikupata jibu,” alisema Asha huku akionekana kuwa na hasira.

Baada ya hapo nilijua kuwa fedha za Wama ni za watu maalum na sio kila mwanamke.
Hata hivyo, Asha alimuomba Mwenyezi Mungu ampe amuweke katika afya njema Rais Kikwete ili aweze kutumia hekima na busara katika uongozi wake; amuepushe na kutumia ubabe na cheo chake katika kuwaongoza Watanzania.

“Uongozi ni dhamana aliyopewa na Mwenyezi Mungu na Mwenyezi: Mungu pia ndiye anayeweza kumnyang’anya dhamana hiyo wala si Watanzania kama anavyodhani, hivyo ajitahidi kuwa mwadilifu, mwenye hekima, busara na imani katika uongozi wake,” alisema Asha.Pia aliwaombea wafanyakazi ambao wanataka kuingia katika mgomo kutofanya hivyo kwa kuwa wakifanya hivyo watadhulumu haki za Watanzania.

“Nawaombea kwa Mungu viongozi wa Tucta wawashawishi wafanyakazi wasigome ili wasibebe dhima ya kudhulumu haki za Watanzania watakaokosa huduma mbalimbali kwa muda wote watakaogoma, Aaaammmiiin,”  alisema Asha ambaye ni mkulima wa kilimo cha jembe la mkono.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Wednesday, 05 May 2010 22:39
 

Comments 

 
0 #187 2011-11-12 17:41
chadema vp aki iko wapi
Quote
 
 
-1 #186 2011-06-15 16:17
Quote:
Ahsante bibi kwa hekima na busara.
Hivi Mh.Rais aliongea na wazee au wanachma wa chama chake? Pili kama hakuna pesa za kulipa wafanyakazi,je zile bilioni za mfuko wa mbunge zinatoka wapi?
Kama wafanyakazi 350,000 watwadhulumu wa tz 40millioni,vipi mafisadi wasiozidi 10 kuwadhulumu 40 milioni.

Ndg yangu kikwete haongei na wazee wa DAR ANAONGEA NA WANACHAMA WENZAKE,Na pia Jamani wazee wetu mnampigia makofi kikwete lakini jueni mkirudi majumbani sisi vijana wenu ambao tunapigania haki yetu ili kunusuru ugumu wa maisha ulipo ndio tunawalea kwa kula yenu kuvaa mpaka matibabu yenu sijui kwanini manashindwa kumbana pindi akiwaita?
Quote
 
 
-1 #185 2011-06-15 16:13
Tutaaanzia wp ndg yangu hii biashsra ya kuwashtakai marais kwa ubadhirifu wa mali ya uma na ukiukwaji wa haki za kibanaadamu tutaishia kuona kwa wenzetu sisi kwetu HAKUNA HICHO KITU N HADITHI MZAZI WANGU,wao wenyewe wamo kwenye hiyo chain Mbuzi wa bwana heri na shamba la bwana heri upo hapo baba
Quote
 
 
-5 #184 2011-03-02 11:31
Quote:
Wewe Mnyika ni mshamba tu na kwa taarifa yako hatukupi kura Ubungo hata kama unachangia kwa kujifichaficha humu..kagombee kwenu Moshi


Tunajua wewe unaomlaumu mnyika ni nambari wani kwa hatujui umemuona mnyika yupo juu unaleta fitina mbona wewe ukugombea ubunge na ukigombea hata mwenyewe utajisahau kujipia kwamaana utapa sifuri
Quote
 
 
+2 #183 2011-03-02 11:24
Quote:
administrator una uwezo wa kukataa barua zenye lugha chafu zisizo ma maana rungu ni lako



Hili ni gazeti la wananchi tuache tutoe maoni yetu kama uwezi wewe soma magazeti ya Habari leo, Uhuru na mzalendo.Maana magazeti hayo ukitoa maoni umetukana serikali hata ujumbe wako uoni kabisa.Big up mwananchi kwa kujali wananchi na maoni yao
Quote
 
 
+2 #182 2011-02-13 18:17
NASIKITISHWA SANA NA WATU WANAO MLAUM DR SLAA, JE AMAN BILA NEEMA INAFAA? NA JE UTANIAMBIA KUWA WEWE UNAAMKA ASUBUHI BILA KUPATA CHAI , CHAKULA HATA CHA KULA CHA JIONI THEN UNASEMA TUAAMANI NI AMAN GANI HIYO?, AJILA NDO AMAN TOSHA, VIONGOZI WETU WALIOPO MADARAKANI ZAIDI YA MIAKA ENZI ZA BABA YETU MPENDWA NYERER WANATENGENEZA AJARA KWA KUWA SOMESHA WATOTO WAO NJE JE WEWE UNASOMA SHULE NA MTOTO WA KIKWETE? AMA KINGUNGE? JIBU UNALO KICHWANI, JAMANI TUSIWE WATU WA KULAUMU MTU MAKINI KAMA DR SLAA., NAMPA HI SLAA, +2550655393831
Quote
 
 
0 #181 2010-10-18 11:22
uwenda sisi watanzania ndo tulivyo ata hayo ya tushinda kuyaelewa wanyakazi tumetajwa kwa idadi kisha kuambiwa kura zate azitakiwi kwanini? tusijongeze
Quote
 
 
-2 #180 2010-09-12 17:12
administrator una uwezo wa kukataa barua zenye lugha chafu zisizo ma maana rungu ni lako
Quote
 
 
0 #179 2010-08-22 10:59
Nasikitika kuona hadi karne hii bado POSTA zetu zina utamaduni wa kufunguwa vifurushi vya wateja vinavyotoka inje ya n'nchi, ukilinganisha na vijin'nchi vichanga kama Rwanda Burundi na kwingineko ukituma parsell kwa jamaa au ktk mashirika binafsi ya huduma za kijamii, vinawafikia bila usumbufu, lakini sio hapa kwetu. JEE!!! WABONGO TUTAAMKA LINI. Simaanishi wabongo wote lakini sifa ya mharibifu m'moja inatugusa sote kwa pamoja. AIBU AIBU AIBU POSTA TZ.
Quote
 
 
+1 #178 2010-05-07 20:18
Quoting Tesha:
Quoting Ndowano:
I can guess with the highest precision as possible that, you have been hired to come up against the sincere folks who utilize their democratic freedom to express their feelings. Do not think that these feelings have been triggered by tribal, religion or political drive, no! If you are true Tanzanian, you don’t need to be taken to school to tell that leadership is the reason. Unless, your bell fully fed from the means ripped off the poor, weak and exploited Tanzanian workers.


And U too! U're hired and paid filthy money by CHADEMA


If your guess is right, take my kudos and be happy brother Tesha. But because I am not a member of Chadema political party, your prognosis is simply another Yahya’s false prophecy...full of unrealistic guesses. Just keep on with your fallacies as your wish.
Quote
 
 
-1 #177 2010-05-07 11:44
Quoting Ndowano:
I can guess with the highest precision as possible that, you have been hired to come up against the sincere folks who utilize their democratic freedom to express their feelings. Do not think that these feelings have been triggered by tribal, religion or political drive, no! If you are true Tanzanian, you don’t need to be taken to school to tell that leadership is the reason. Unless, your bell fully fed from the means ripped off the poor, weak and exploited Tanzanian workers.


And U too! U're hired and paid filthy money by CHADEMA
Quote
 
 
-1 #176 2010-05-07 11:41
You Ndowano det har tagits fram ett underlag för vindkraftsplane ring, som pekar ut områden som bedömts möjliga för vindkraftver ketablering. Stop your filthy mouth against our national peace and tranqulity...Go to school again!
Quote
 
 
+2 #175 2010-05-06 17:48
But I can assure you, the bell is ringing, time is over, change is galloping to take its place. Keep on smiling now, but in next to no time you will be crying, because the time for the poor to smile is come. I have no quarrel with you, I go home to eat ugali wangu na kauzu, while you enjoy your bear n your kids a good meal/dinner.
Quote
 
 
+2 #174 2010-05-06 17:46
I can guess with the highest precision as possible that, you have been hired to come up against the sincere folks who utilize their democratic freedom to express their feelings. Do not think that these feelings have been triggered by tribal, religion or political drive, no! If you are true Tanzanian, you don’t need to be taken to school to tell that leadership is the reason. Unless, your bell fully fed from the means ripped off the poor, weak and exploited Tanzanian workers.
Quote
 
 
+3 #173 2010-05-06 17:45
Ustaadhi and Mkata ngebe, please leave me a free Tanzania to air my comments without restraint. Nobody asked me to give out my comments; I’m doing so out of my jingoistic feelings for my beloved country. Tanzania, not parties, is my mother and I am compelled to love and defend her even if my weapon is just a prayer to the God above. Bi Aisha did the same, why not me? I hope her prayer has been heared.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner