
| Lowassa apata kikombe Loliondo | Send to a friend |
| Tuesday, 15 March 2011 23:47 |
|
Waandishi Wetu Tofauti na viongozi wengine, Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), Jimbo linalopakana na Kijiji cha Samunge, alikwenda huko akiwa na viongozi mbalimbali wakiwamo viongozi wa dini na baadhi ya wapigakura wake. Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Lowassa alithibitisha kwenda Loliondo na kuwataja viongozi wa dini alioambatana nao katika msafara wake kuwa ni Askofu Msaidizi wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini, Dk Frederick Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Dayosisi ya Kaskazini Kati (Arusha), Mchungaji John Nangole. Katika ramani ya utendaji kazi ya KKKT, Jimbo la Masai Kaskazini ndipo kilipo Kijiji cha Samunge ambako ni makazi ya Mchungaji Mwasapile.“Ni kweli, nimekwenda pale na wapigakura wangu pamoja na viongozi wa dini, Msaidizi wa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Dk Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Mchungaji Nangole,” alisema Lowassa na kuuliza: “Kwani hiyo nayo ni habari jamani?” Baada ya Lowassa kufika katika kijiji hicho akiwa na ujumbe wake, aliongoza moja kwa moja hadi kwa Mchungaji Mwasapile na kuzungumza naye kisha akapata kikombe cha tiba na kuondoka.
Habari zilizopatikana hospitalini hapo jana zimeeleza kuwa wagonjwa hao walianza kuondoka Muhimbili juma lililopita baada ya Serikali kubariki matibabu hayo. Ofisa mmoja mwandamizi wa hospitali hiyo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe gazetini, amesema kuwa wakati baadhi ya wagonjwa hao wakiwa wanatoroka wodini, wengine wamekuwa jasiri kwa kuwaaga madaktari wao. “Wagonjwa wameanza kuondoka na wengine bila hata ya kuaga, hivyo hatujui hatima yao kama watafika salama huko Loliondo,” alisema.Ofisa huyo alisema juma lililopita, mgonjwa mmoja aliyekuwa amelazwa chumba namba 15 katika Wodi ya Kibasila, aliondoka baada ya kusikia taarifa kuhusu huduma hiyo. “Kuna mgonjwa mmoja aliyekuwa amelazwa Kibasila Wodi namba 15 aliondoka aliposikia kuwa Babu ameanza tena kutoa matibabu hayo ambayo awali yalisitishwa,” alisema.Hata hivyo, Ofisa Habari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Aligaisha alisema hana taarifa za kutoroka wodini kwa wagonjwa hao na kwenda kufuata tiba huko Loliondo... “Sina taarifa zozote za kuondoka kwa wagonjwa hapa hospitalini.” Mmoja wa mawakala wa mabasi ya abiria katika kituo hicho ambaye hakutaka kutajwa gazetini alisema ongezeko hilo la nauli limetokana na baadhi ya mawakala kukodi mabasi na kuwasafirisha abiria.“Nikupe siri moja tu ambayo inatufanya tupandishe nauli. Lengo letu ni kupata faida, ujue sisi tunakodi basi zima kisha tunakatisha tiketi kwa bei yetu ili na sisi tupate faida,” alisema. Kwa mujibu wa abiria huyo, zamani nauli za Arusha zilikuwa Sh25,000 kwa basi la daraja la juu, Sh18,000 kwa mabasi ya daraja la kati na Sh15,000 kwa daraja la chini, lakini sasa mabasi yote yanatoza kati ya Sh25,000 hadi Sh30,000.“Mawakala hawa wanadhani kila mtu anayepanda magari haya anakwenda Loliondo lakini siyo kweli, wengine tuna safari nyingine kabisa," alisema Manyama na kuongeza: Hatua ya polisi kuonekana katika kituo hicho, ilisababisha wasiwasi kwa wananchi kuwa huenda Serikali imesimamisha utaratibu wa wananchi kwenda Loliondo, jambo ambalo kaimu kamanda huyo alilikanusha. Wananchi waliozungumza na gazeti hili bila kutaja majina yao walisema kuwa wanashangazwa na bei ya nauli kuwa juu hata baada ya Serikali na KKKT, Dayosisi ya Kaskazini Kati kuboresha mazingira ya kuwahi kupata tiba na kuondoka kijijini Samunge. Habari hii imeandaliwa na Nevile Meena, Ibrahim Yamola, Dotto Kahindi Dar na Mussa Juma, Filbert Rweyemamu, Arusha |
| Last Updated on Thursday, 17 March 2011 07:39 |

Habari Mpya
Picha
Zenye Mvuto
- Prof Mwandosya aapishwa waziri kazi maalum
- Katiba Mpya: Wananchi Makambako waapa, iwe jua au mvua lazima watoe maoni yao
- Mchakato wa Katiba: Nahodha yupi aaminike? 1
- Wanavyosema wanasiasa kuhusu Katiba mpya
- Serikali inasita nini kutumia Kiswahili kufundishia shule za sekondari?
- Jamii inaweza kuleta mabadiliko katika elimu
- Nafasi za Kazi
- Links za wateja na washirika wetu
- Muswada wa madini waitoa jasho serikali
- Bi kizee asafari kilometa 50 kupinga hotuba ya JK, AMUONYA ASITUMIE MADARAKA YAKE VIBAYA
- Mishahara sekta binafsi Tucta yashtukia danganya toto
- Vigogo UVCCM wajiuzulu
- Mwinyi atetea ajira za wafanyakazi, ashauri utu uheshimiwe kudumisha Amani















Comments
we ngedere jiheshimu kabisaaaaaa,ten a uchunge huo ulimiwako mkali kama wa ndege,soma vizuri mahubiri aliyoota Pengo,alisema KAMA MAANDAMANO YA CHADEMA BAADA YA UCHUNGUZI YAKIONEKANA YANAWEZA KULETA MADHARA BASI YADHIBITIWE,sas a unataka kusema anamtetea Slaa hapo? pu mba vu kabisa wewe soma vizuri uelewe habari na sio kupapatikia tu kama kinda la bundi!! halafu hakuna Padri aliyepinga huduma ya Babu,pia,Pengo ameonesha wasiwasi tu kuhusu hiyo huduma,hajasema haina ukweli,we ngedere jiheshimu na usome kwa kuelewa usirukie rukie tu.
MMEKOSA MAMBO MUHIMU YA KUANDIKA JAMANI? MAGAZETI YA UDAKU YAANDIKE NINI SASA KAMA MNAANDIKA MAMBO YASIYO NA MANUFAA YEYOTE KWA JAMII,,JAMANI TUNAMAMBO MENGI YA KUANDIKA KAMA HUU UKURASA HAUNA CHA KUANDIKA NAOMBENI MNIPE MIMI KAZI NIWAPE MAMBO YA MSINGI MUANDIKE...
tunataka kuona waliofika, wenye afya mbofumbofu na wenye kijifanya wazima kumbe wabovu,na zaidi kuweka kumbukumbu...tena ikiwezekana uwe unatwanga na picha kabisa.la mwisho, wapige mkwara, wasipotengeneza barabara na kuweka taa njiani na ikiwezekana lami..basi unasitisha zoezi zima na kila kiongozi aliyekunywa dawa ,ambae kwa namna moja au nyingine anazorotesha maendeleo ya nchi, ile dawa haitafanya kazi ,na itakuwa sumu mwilini na unatoa simu 30 tu.
lowasa saiv ni mwema?