MwanzoContactsEmail
Home Jumapili Biashara Mtaalamu asisitiza mafuta yamepatikana
BOOKMARK THIS PAGE
Mtaalamu asisitiza mafuta yamepatikana  Send to a friend
Saturday, 19 June 2010 21:28

Mwandishi Wetu
MTAALAAMU wa kimataifa wa nishati amesema, upatikanaji wa mafuta nchini Tanzania  umefikia katika hatua za kuridhisha. Katika mahojiano na gazeti hili jana, Dk Philip Nelson, alisema mafuta na gesi  sasa yanapatikana katika mfumo mpya wa kutumia bahari. Alisema Februari 2008, Kampuni za Petrodel Resources Limited (PRL) na Heritage Oil Limited, kwa pamoja walifanya uchunguzi katika bahari, magharibi ya Visiwa vya Mafia.
 
 “Nilikuwa na uhakika  kuwa naona DHIs katika taarifa zilizohifadhiwa TPDC, hivyo kwa msaada wao, tuliweza kutengeneza karatasi safi tulizozichapisha kutoka katika filamu ya TPDC. Baada ya hapo, tukabadilisha picha  kwa mfumo wa  kitaalamu na kuzihamisha taarifa hizo kwa kompyuta maalumu ili kupata picha nzuri zaidi," alisema Dk Nelson. Hata hivyo, alisema mbali ya hapa Tanzania alifanya kazi ya utafiti kwa miaka mitatu nchini Nigeria akifanya katika kampuni ya mafuta ya Petroleum Development. Alisema kuwa maeneo yenye visima hivyo yanapatikana huko Latham, Kimbiji. Mtafiti huyo alisema visima vimefikia urefu wa mita 3,500 baada ya kuchimba mzunguko ambao ni sawa na asilimia 90.
 
“Visima vimefikia urefu wa kiasi cha meta 3,500, baada ya kuchimba kwa mzunguko sawa wa asilimia 90, hali ni nzuri kwa mabwawa ya miamba kwa ajili ya kukusanya mafuta,  lakini hakuna kifungo cha kuzuia mafuta yatakayopita katika mzunguko huo” alisema Dk Nelson. Alisema, Petrodel imedhamiria kutafuta na kuzalisha mafuta na gesi kwa manufaa ya Watanzania.
 
‘Tanzania, ni nchi nzuri yenye watu wazuri na wakarimu, nina bahati kubwa kukutana nanyi ni sehemu nzuri kufanya kazi na Rais ametengeneza mazingira yanayowezesha biashara bora,” alisema Dk Nelson. Mtaalamu huyo aliongeza kuwa,Desemba 2008,  kampuni ilipata eneo la kilometa 1,200, za mafuta katika bahari na kwamba taarifa hizo zimeonyesha hali ya kuridhisha  ya upatikanaji wa mafuta na gesi. Dk Nelson ni mtafiti wa mafuta mwenye ujuzi wa karibu miaka 45 katika sekta za viwanda na gesi. Vilevile alifanya  kazi hiyo katika kampuni ya utafiti wa mafuta nchini Uingereza kwa miaka 6.       


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
+1 #5 2012-02-22 00:46
Kampuni za Petrodel Resources Limited (PRL) na Heritage Oil Limited, kwa pamoja walifanya uchunguzi katika bahari, magharibi ya Visiwa vya Mafia.
sidhani kama ni magharibi mwa visiwa vya mafia bali ndani ya visiwa vya zanzibar kwa hiyo hakuna mwisho mwema kwa maana wazanzibar hawataki mafuta yawe ya muungano
Quote
 
 
+3 #4 2010-08-22 09:56
Tanzania ina maliasili nyingi hata hivi sasa kabla ya mafuta hayo.Swali ni kwamba zimetusaidia vipi kukuza uchumi wetu.Sera za wizi wa makusudi na wazi wazi za viongozi walioko madarakani zinatufanya tuendelee kudidimia.Tunahitaji kubadili mfumo mzima wa uongozi ili tuweze kupata viongozi wenye uchungu na Nchi yetu na si hawa waroho wazee wa Vijisenti wanaolindana kuinyonya nchi yetu na kutulazimisha kuwa masikini bila sababu!MUNGU IBARIKI TANZANIA!
Quote
 
 
+3 #3 2010-07-14 18:30
Hata zingenguliwa tani za zillions za dola bado haziwezi kuwafaa wadanganyika kwa aina hii ya majambazi na majizi waliojazana madarakani.
Kwa madini na raslimali nyingine nyingi tulizo nazo, tungekuwa na watawala wanaotumia common sense tu, tungekuwa kama Botswana. Utajiri bado utapatikana na wahindi watauhamishia India.
Quote
 
 
+2 #2 2010-07-03 19:11
Maoni yangu hayo mafuta ni bora yasipatikane, maana kwa uzembe wa viongozi wetu hayatawasaidia wananchi hata kidogo. Angalia shinyanga mkoa una madini mengi, lakini masikini sana. Wananchi wazingatie umuhimu wa kura zao ili wafaidike na maliasili yao, wasikubali kudanganywa.
Quote
 
 
+5 #1 2010-07-02 22:14
Mimi namshukuru sana Mungu kwa hatua hiyo iliyofikiwa na watafiti wetu Dk Nelson.
Sasa sakata liko kwa viongozi wa nchi yetu.
Je,wananchi watanufaika kwa jinsi yoyote ile katika hatua hii ya kuwa na visma vyetu wenyewe?Hadi sasa tuna visima vya kutosha vywa gasi tukitegemea kushuka kwa kiwango cha mwananchi wa kawaida kumudu kutumia gasi badala ya kuni na kunsuru janga la jangwa nchini;lakini bado matumizi ya gasi kwa mwanach wa kawaida ni njozi.nchi jirani zatumia gasi yetu kwa bei nafuu kuliko TANZANIA.Tunaomba miujiza kutoka kwenu ,Waswahili hema,Mcheza kwao hutunzwa.NCHI NYINGI ZENYE UWEZO NI ZILE ZINAZOWAJALI WANANCHI WAKE KWA KUHAKIKISHA KILE KINACHOPATIKANA NCHINI KINABAKI NCHINI.HATA HAO WANAOTULETEA MISAADA HULETA WATU WAO NCHINI NA WAWAAJIRI KWA PESA HIZOP ZA MISAADA wanazotudangany a nazo.mimi.....sijui
mdau
Moro.
Had
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner