
| Mkakati wa kuwang'oa Sitta, Makinda waiva | Send to a friend |
| Saturday, 01 May 2010 22:32 |
|
Sadick Mtulya MKAKATI uliosukwa kuwang’oa baadhi ya wabunge katika majimbo yao unaodaiwa kusukwa na kigogo mmoja ndani ya CCM, umeanza kutekelezwa, imebainika. Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa mpango huo una lengo la kuwaondoa baadhi ya wabunge wanaonekana ni kikwazo kwa kigogo huyo ndani ya bunge kufanikisha malengo yake, ili bunge lijalo liwe na sura mpya. Niongoni wa wanaotakiwa kungolewa ni akiwemo Spika wa Bunge, Samuel Sitta na Naibu wake, Anna Makinda pamoja na wabunge wengine. Tayari mpango huo umeaanza kutekelezwa kwa kuwawekea wapinzani katika majimbo yao ambao wana uwezo wa fedha na wengine wanawekewa wapinzani wawili au zaidi ili kuhakikisha wanashindwa katika kura za maoni ndani ya CCM. Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili unaonyesha kuwa tayari wabunge hao akiwamo Spika Sitta wamegundua hujuma hiyo na sasa wanajipanga kupambana na watu hao. Hata hivyo, wabunge hao wameaamua kulifikisha suala hilo kwa Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa taifa CCM kuomba wahakikishiwe kama hujuma hizo zina baraka ya chama. Taarifa zinasema kuwa mmoja ya wabunge hao alimfuata Rais Kikwete wakati wa mkutano wa 18 wa bunge mjini Dodoma mbele ya wabunge waliokuwa wameudhuria kwenye hafla ya jioni kuhoji kama chama kinajua mkakati huo. Inadaiwa kuwa Mbunge huyo alimuuliza Rais Kikwete kana ni kweli kuna watu wametumwa na chama wakagombee ubunge kwenye majimbo wanayowakilisha, ili wasigombane. Hata hivyo, taarifa zinasema kuwa baada ya swali hilo, Rais Kikwete alishtuka na kulazimika kwendakwenye kipaza sauti ili wabunge wote waliokuwepo na kusisitiza kwamba, hajamtuma mtu yoyote majimboni. Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana, Spika Sitta alikiri kusikia kuwepo kwa taarifa za mpango wa kung’olewa pamoja na Makinda na baadhi ya wabunge. Hata hivyo, Sitta alisema mkakati huo ni sehemu ya mapambano ya siri yanayoendeshwa chini kwa chini dhidi yao. “Pamoja na kwamba nipo jimboni hivi sasa, nimesikia kuwa mimi, Makinda na wabunge kadhaa tung’olewe,” alisema Sitta na kuongeza: "Lakini yote haya ni sehemu ya mapambano ya siri yanayoendeshwa chini kwa chini dhidi yetu”. Sitta alifafanua kwamba, mpango huo umewekwa dhidi yao kutokana na utendaji wao bungeni na kwamba wataendelea kupambana na hali hiyo. “Kutokana na utendaji wetu bungeni, mimi na Naibu Spika tulijua hili litajitokeza, lakini tutendelea kupambana na hali hii,” alisema Sitta. Sitta alisema pamoja na mambo mengine wananchi pamoja na wana-CCM ndiyo watakaoamua hatma yao na si vinginevyo. Alisema walioanda mpango wa kuwang’oa ni watu wenye ajenda ya chuki na gadhabu ambazo hazina msingi wowote katika maendeleo ya nchi. Sitta alibainisha kuwa pamoja na watu hao kutumia fedha nyingi, hawatafanikiwa. “Hawa watu wana ajenda ya chuki na gadhabu ambazo hazina msingi wowote katika maendeleo ya nchi,” alisema Sitta. Sitta alijitapa kuwa hana wasiwasi na nguvu zinazotumika kumg’oa na kusititiza kwamba, atashinda katika uchaguzi mkuu wa Oktoba. “Siku zote wananchi wanaangalia jinsi Mbunge alivyosaidia katika shughuli mbalimbali za kuwaletea maendeleo yao pamoja na ya taifa. Hata watumie fedha kiasi gani, mimi sina wasiwasi na nitashinda,” alisema. Sitta aliwaonya watu wanaotaka kumng’oa kuwa majibu ya jinsi anavyokubalika wangeyapata kupitia taasisi ya utafiti wa Demokrasia na Elimu nchini(Redet) kama ingefika kufanya utafiti katika jimbo lake. “Bahati yao utafiti wa Redet haukupita katika jimbo la Urambo Mashariki, wangepata majibu yao na wangejua mimi ni nani,” alisisitiza Sitta. Juhudi za kumpata Makinda hazikuza matunda alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi. Naye Mbunge wa Jimbo la Mchinga(CCM), Mudhihir Mudhihir ambaye ni mmoja wa wabunge waliotajwa kuwa walengwa wa mpango huo wa kung’olewa, alisema katika uchaguzi waamuzi ni wananchi. “Katika jimbo la Mchinga wapo wagombea wanane ambao wameletwa, lakini ninachosema ni kwamba, wananchi ndio waamuzi katika uchaguzi wowote,” alisema Mudhihir Mbunge huyo alisema pamoja na kwamba yupo tayari kupambana nao, lakini katika kupata ubunge hakuna ujanja na kwamba wote walituomwa kwa ajili ya kumuhujumu wataumbuliwa na Mungu. “Mimi nitagombea na nipo tayari kupambana nao, lakini, naamini Mungu atawaumbua tu kutokana na nia zao mbaya,” alisema Mudhihir . Kutoka Ruvuma, Joyce Joliga, anaripoti kuwa Tasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Ruvuma inamshikilia mpambe wa mmoja vigogo wa (CCM) baada ya kukutwa akigawa rushwa kwa mabalozi 50 wa Kata ya Majengo, Songea mjini. Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana katika Kata ya Majengo, ambako mpambe huyo (jina tunalo) alikamatwa akiwa nyumbani kwa mmoja wa wajumbe wa shina pamoja na mabalozi 50 kwa lengo la kuwapa Sh 2,000 kila mmoja. Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Ruvuma, Daudi Masiko alikiri kuwepo kwa tukio na kwamba taarifa kamili itatolewa kesho. |

Habari Mpya
Picha
Zenye Mvuto
- Prof Mwandosya aapishwa waziri kazi maalum
- Katiba Mpya: Wananchi Makambako waapa, iwe jua au mvua lazima watoe maoni yao
- Mchakato wa Katiba: Nahodha yupi aaminike? 1
- Wanavyosema wanasiasa kuhusu Katiba mpya
- Serikali inasita nini kutumia Kiswahili kufundishia shule za sekondari?
- Jamii inaweza kuleta mabadiliko katika elimu
- Nafasi za Kazi
- Links za wateja na washirika wetu
- Muswada wa madini waitoa jasho serikali
- Bi kizee asafari kilometa 50 kupinga hotuba ya JK, AMUONYA ASITUMIE MADARAKA YAKE VIBAYA
- Mishahara sekta binafsi Tucta yashtukia danganya toto
- Vigogo UVCCM wajiuzulu
- Mwinyi atetea ajira za wafanyakazi, ashauri utu uheshimiwe kudumisha Amani















Comments
Wewe Bwana mdogo huna nidhamu, mimi nilikuwa Waziri Mkuu nikakubali kujiuzulu na ninaipenda CCM hadi kufa, kwa nini inahimiza watu wengine kupigia chama ya upinzani? Tafadhali usifanye kampeni kupitia forum hii, nimekuona na nitakushughulik ia.
Demokrasia kwao ni maneno tu lakini mioyoni mwao usultani/ufalme umekithiri. Hii habari ya kujifanya eti wao ni watendaji wazuri ndo maana inapangwa mikakati ya kuwang'oa haina mantiki hata kidogo. Wnananchi ndo wenye uwezo wa kupima utendaji wao na si kujipigia debe. Kama wangekuwa watendaji wazuri wasingeruhusu uozo wakati wa mijadala ya Richmond, EPA n.k. Wamefanikiwa kucheza sinema wakijifanya sterling wa kihindi. Shame on you - all bogus politicians!
Hivi hao akina Sitta, Makinda wana leseni ya kukaa kwenye majimbo yao hadi lini? Kwa nin wahoji uhalali wa watu wengine kugombea majimboni mwao? Hawana hata aibu kuongea hadharani eti watu wametumwa kuja kuwang'oa ili kufanikisha malengo ya mafisadi, kwani demokrasia ni nini kama hawataki ushindani?
Haya na huo ufisadi wanaojifanya wanapingana nao ni upi, maana kila atakapoongea Sitta anasema mafisadi wanafanya njama wamng'oe jimboni kwake. Inamaana kila anayegombea amekuwa fisadi? Labda neno fisadi limebadili maana yake atuambie vizuri lakini sio kulitumia katika kujitangaza.
Na nyie waandishi na wahariri kuweni makini jamani, msituchanganye wasomaji na siasa zenu. Hili wala halihitaji elimu kubwa kama za kiwango cha shahada kulielewa.