MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Kitaifa Mkulo: Uchumi unazidi kukua
BOOKMARK THIS PAGE
Mkulo: Uchumi unazidi kukua  Send to a friend
Saturday, 29 May 2010 09:22

Exuper Kachenje
SERIKALI imesema kuwa ukuaji wa pato la taifa katika unakadiriwa kuongezeka na kwamba pato halisi litakua kwa asilimia 7 katika mwaka 2010.
 
Akiwasilisha taarifa ya mwelekeo wa uchumi kwa mwaka 2009 na mwelekeo katika kipindi cha kuanzia 2010 hadi 2013 mbele ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo alisema kuna matarajio makubwa uchumi kuendelea kukua.
 
Huku akiwaomba radhi wabunge kwa kuchelewa kuwapa nakala ya taarifa hiyo, Mkulo alisema maelezo hayo yalipitishwa juzi asubuhi na Baraza la Mawaziri.
 
"Naomba radhi waheshimiwa kwa kuchelewa kuwapatia nakala ya taarifa hii kwa kuwa imepitishwa jana asubuhi (juzi) na Baraza la Mawaziri hivyo imechelewa kuchapwa,"  Mkulo alisema.
 
Mkulo alisema kuwa katika mwaka 2011, pato halisi la uchumi litakuwa kwa asilimia 7.1, mwaka 2012 asilimia 7.4 na hadi kufikia mwaka 2013 pato halisi la taifa litafikia asilimia 7.8.
 
“Kama ilivyotarajiwa athari za msukosuko wa uchumi zilikuwa za mpito, hivyo ukuaji wa pato la taifa unakadiriwa kuanza kuongezeka. Pato halisi litakua kwa asilimia 7.0 mwaka 2010, asilimia 7.1 mwaka 2011, asilimia 7.4 mwaka 2012 na kuendelea kuongezeka hadi asilimia 7.8 mwaka 2013,” alisema Mkulo.
 
Alifafanua kuwa malengo hayo yanatarajiwa kufikiwa kwa kutekeleza sera na misingi ya uchumi kwa kuzingatia mambo mbalimbali, ikiwemo mwenendo wa uchumi wa dunia na hitaji la kujenga uwezo kukabiliana na athari za msukosuko wa uchumi wa dunia.
 
Alitaja misingi mingine kuwa ni kuendelea kutengemaza vigezo muhimu vya uchumi jumla na maendeleo ya jamii hasa mfumuko wa bei, kuweka msukumo katika utekelezaji Dira ya Maendeleo ya Taifa, Mkukuta awamu ya pili, Kilimo Kwanza na kuelekeza rasilimali kwenye maeneo chochezi ya uchumi kwa haraka zaidi.
 
Kwa mujibu wa Mkulo katika kipindi hicho miradi inayopewa kipaumbele katika mwongozo huo wa bajeti itakuwa ni pamoja na miundombinu, uendelezaji ardhi na makazi pamoja na vitambulisho vya taifa.
 
Vingine ni nishati, viwanda, sekta ya fedha na pia kutaja uchaguzi mkuu ujao wa Oktoba mwaka huu kuwa ni kipaumbele cha kipekee kwa serikali katika mwaka huu kwa lengo la kuhakikisha unafanyika kama ilivyopangwa.
Waziri huyo alisema katika muda huo kasi ya upandaji wa bei inakisiwa kupungua hadi asilimia 8.0 kufikia mwezi Juni mwaka huu na kupungua zaidi hadi asilimia tano ifikapo Juni 2011.
 
Aidha, alisema katika kipindi hicho mapato ya ndani  ya taifa yatafikia uwiano wa asilimia 17.3 kwa mwaka 2010/11; asilimia 17.4 mwaka 2011/2012 na asilimia 17.6 ifikapo mwaka 2012/2013.
 
Alisema serikali pia inalenga kuwa na akiba ya fedha za kigeni itakayokidhi uagizaji bidhaa kutoka nje na huduma kwa kipindi kisichopungua miezi mitano; kuwa na viwango imara vya ubadilishaji wa fedha; kuboresha mazingira ya uwekezaji na kufanya biashara na kuedeleza kilimo na kupunguza viwango vya riba.
Kuhusu biashara, Mkulo alisema Tanzania imeshuka katika vigezo vya urahisi wa kufanya biashara kutoka nafasi ya 126 kati ya nchi 183 na kuwa ya 131 mwaka 2009.
 
Kuhusu mapato  ya ndani, Waziri Mkulo alisema yaliongezeka kwa asilimia 18.1 kufikia Sh4,293.1 bilioni mwaka 2008/09; kutoka Sh3,634.6 bilioni mwaka 2007/08 na kwamba kiasi hicho ni pungufu ya asilimia 10 kwa mwaka 2008/09.
 
Kwa kipindi cha Julai 2009 hadi Machi 2010, mapato ya ndani yalifikia Sh3,490.3 bilioni ikiwa chini ya asilimia 8.7 ya makisio ya Sh3,924.9 kwa kipindi hicho akieleza kuwa hali hiyo ilitokana na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia.
 
Mkulo alisema kwa kipindi cha Julai 2009 hadi Machi mwaka huu matumizi ya serikali yamefikia Sh6,143.9 bilioni kati ya makisio ya Sh6,718.7 kwa kipindi hicho, ikiwa ni upungufu wa asilimia tisa uliotokana na upungufu wa mapato.
 
Wakichangia maelezo hayo wabunge walitaka serikali ieleze itafanya nini kuwezesha wananchi kumiliki uchumi badala ya kumiliki asilimia 10 pekee kama ilivyo sasa.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #12 2010-05-31 10:01
;-) kwa kweli m imi kama mtanzania sioni umhimu ya ukuaji huo wa uchumi wa bongo angali huduma za kiafya, miundombinu mijini dhamani ya shilingi dhidi dola, elimu na ajira vyazidi kudorora! Hizo ni takwimu tu zisizo zinazobamba vyombo vya habari tu.
Quote
 
 
0 #11 2010-05-31 08:33
Mkulo alisema kwa kipindi cha Julai 2009 hadi Machi mwaka huu matumizi ya serikali yamefikia Sh6,143.9 bilioni kati ya makisio ya Sh6,718.7 kwa kipindi hicho, ikiwa ni upungufu wa asilimia tisa uliotokana na upungufu wa mapato....Kwa maoni yangu taarifa kama hizi zingetolewa kwa wakati kwani tulio wengi na hasa kupitia taarifa kwennye vyombo vya habari tulielewa kuwa serikali imetumia zaidi ya makisio yake.Naje hali matumizi yakoje kwa Aprili Desemba 2009? Taarifa hizi zitanisaidia kuamini ama kuacha kuamini yaliyokwishajir i kwenye vyombo vya habari
Quote
 
 
0 #10 2010-05-31 07:54
Kweli Tanzania yetu ina viongozi wa ajabu:

Uchumi gani unakuwa kwa mambo yafutayo:

1. inflation toka 5.3%- 9.6%??
2. Tax revenue kushuka kwa 30%?
4. Government spending kuwa juu ya collection?
5. Export kushuka kwa karibu 40%?
6. Exchange rate Tsh 1500 kwa dola moja?
7. Major economic means industries, banking, mining, tourism, kuwa mikononi mwa wageni ambao faida yote wanapeleka kwao?

Tunadanganywa kama watoto; tuamke!!!!!
Quote
 
 
0 #9 2010-05-30 08:23
hivi ni lini wananchi tutakuwa na uwezo wa kusimamia kile tunachokitaka toka kwa serikali iliyo madarakani,inau ma sana kila ninaposoma na kusikia habari za uongo kwenye vyombo vya habari kuhusu nchi yangu,eti uchumi unatarajiwa kupanda kwa 7% ilihali hakuna hata mikakati madhubuti kuthibiti ushukaji wa thamani ya pesa yetu,kweli shilingi inakaribiana na pesa ya Uganda leo hii kwa tofauti ya desimali kadhaa????ni lini hawa watu tunaowaamini kuwapa dhamana ya kutuongoza wataacha siasa na kusimamia maslahi ya Taifa?
Wakati wengine wanapiga hatua mbele sisi ni kama tunarudi hatua mara dufu nyuma...
Mungu ibariki Tanzania!
Quote
 
 
0 #8 2010-05-29 20:13
SWALI KWA WACHUMI,
Kwa kuwa uchumi wa nchi kwa mujibu wa mkulo unakuwa kwa asilimia 7.1 na inflation yetu ni asilimia 12 hii aimaniishi kuwa uchumi umeshuka(12-7.1=4.9) kwa asilimia 4.9????.
pili kama pato letu la ndani ni 4.2 trillioni mwaka 2008/9. na budget ilikuwa almost 10 trillioni, hii inamaanisha pato letu la ndani linaisha ndani ya miezi6 tu na inamaanisha miezi6 iliyobaki ni ya kukopa?? naomba majibu kwa wale ndugu zangu wachumi wa gazeti hili au watoa maoni na nini tufanye kuondokana na hili maana inaonyesha nchi yetu ni kama Bankcrupty!
Quote
 
 
0 #7 2010-05-29 18:03
wabunge wangu nawapongeza sana na nina waunga mkono kwamba nimuhimu sasa serikali yetu itambue kwamba watanzania wanahitaji kumiliki uchumi wao,tofauti na ilivyo sasa kwamba 90%inamilikiwa na wageni,chakufan ya ni>kuwawezesha watanzania kumiliki viwanda,kumilik i migodi mikubwa ya madini,kuwaweze sha wakulima wakubwa kwa wadogo,kuvibana vyombo vya fedha ili viwepo kwa mtazamo wa kukuza uchumi wa taifa tofauti na sasa kwamba vipo kibiashara zaidi,kuwabana wawekezaji wanje kuakikisha kwamba ni wawekezaji kweli na sio wababaishaji ambao baadae wanakuwa mzigo kwa taifa,pia kuwe na masharti yanayo wataka wawekezaji kuwa na hisa zinazo lingana na wazawa,kwamba mwekezaji ili akubaliwe kuwekeza sharti aonyeshe na kuthibitisha ushiriki wa mtanzania halisi ndani ya uwekezaji wake. waheshimiwa wabunge na serikali yetu haya ya kizinga[NENO BAYA] tunaweza kuanza kumiliki uchumi wetu angalau 50%.
Quote
 
 
0 #6 2010-05-29 16:25
Lugha ya kukua kwa uchumi inaeleweka bungeni,na kwa wajanja wachache waliokaa mkao wa kula, na labda kwa REDET. Lakini si kwa Mtz wa kawaida ambaye maisha yake yanazidi kuwa duni kila kuchapo. Naweza kuwa "green" katika lugha ya uchumi lakini thamani yetu ya fedha inayoshuka kila siku hata inazidiwa na vinchi ambavyo vimekuwa vitani miaka nenda rudi na tegemeo lao ni kilimo cha chai tu, au kahawa, hainishawishi kuamini maneno ya Mh. Mkulo. Tafsirini kukua kwa uchumi kwa kupima maisha ya Mtz na nguvu ya sarafu yenu. Vinginevyo hiyo itabaki longolongo tupu.
Quote
 
 
0 #5 2010-05-29 13:41
Mkulo: Uchumi unazidi kukua

Wafadhiri: fedha tunazotoa haziendi ktk miradi na kusababisha umasikini uliokifiri hivyo tumesitisha zaidi ya bilioni 200 kuipa serikali ya tz

Swali: Inakuwaje tukijihakiki wenyewe tunajipa POSITIVE RESULT na wakituhakiki wafadhili wanatupa NEGATIVE RESULT?

Mimi: ha! ha! ha!
Quote
 
 
0 #4 2010-05-29 12:53
Mmmmh, hizi nii ndoto gani tena hizi, mbona hizi hadithi ni ngumu kuzielewa jamani. Mkulo umetumia vigezo vya kinadharia kuliko vya uhalisia...hivi gharama za maisha kupanda ndo tunamaanisha uchumi unakuwa? ladda mnisaidie jamani.
Quote
 
 
0 #3 2010-05-29 11:32
Mkulo hafai kuwa Waziri wa fedha yaelekea amegushi cheti.Kwa nini anadanganya Watanzania kuwa uchumi umekuwa wakati dola moja ni shilingi 1,500/= za Tanzania. Ingekuwa dola moja ni shilingi 500/= ningekubali uchumi umekuwa.Anamdanganya nani sasa!
Quote
 
 
0 #2 2010-05-29 11:29
Mkulo is nothing. He is killing us. He hasnt the qualifications for that too big post. Better he steps down before things get worse.
Quote
 
 
0 #1 2010-05-29 10:28
DAAH HIVI HUYU ANAESEMA UCHUMI UMEKUA,LABDA UCHUMI WA FAMILIA YAKE LAKINI KWA WATZ TULIO WENGI STILL BADO MAISHA MAGUMU
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner